WACHEZAJI
wawili majeruhi wa Manchester United, Ashley Young na Cameron
Borthwick-Jackson wako fiti kuelekea mchezo wa kesho wa Europa League
dhidi ya mahasimu, Liverpool baada ya kupona maumivu yao.
Young
amerejea mazoezini baada ya miezi miwili ya kuwa nje na leo amefanya
mazoezi wakati Manchester United ikijiandaa kwa mechi ya Europa League
dhidi ya Liverpool Uwanjawa Old Trafford kesho usiku.
WInga
huyo wa England hajaonekana uwanjani tangu United iifunge Liverpool 1-0
Uwanja wa Anfield Januari 17 baada ya kwenda kufanyiwa upasuaji
Marekani kutokana na matatizo ya nyonga
Nahodha Wayne Rooney, Phil Jones, Luke Shaw na Will Keane sasa wanabaki kuwa wachezaji pekee majeruhi, baada ya Cameron Borthwick-Jackson pia kufanya mazoezi leo asubuhi Uwanja wa Carrington.
Borthwick-Jackson hajacheza tangu United iifunge 3-0 Shrewsbury katika Kombe la FA February 22.
Kikosi cha Louis van Gaal kilionekana kipo vizuri kuelekea mchezo huo ambao wanahitaji kukipiku kipigo cha 2-0 walichopewa wiki iliyopita Uwanja wa Anfield kwa mabao ya Daniel Sturridge na Roberto Firmino ili kwenda Robo Fainali.
0 comments:
Post a Comment