Home » » LIGI KUU BARA YAZIDI KUNOGA,MECHI MOJA KUPIGWA LEO MKWAKWANI

LIGI KUU BARA YAZIDI KUNOGA,MECHI MOJA KUPIGWA LEO MKWAKWANI


 
RATIBA LIGI KUU YA VODACOPM TZ BARA
Machi 14, 2016
African Sports Vs Mbeya City
Machi 16, 2016
Azam FC Vs Stand United
Machi 18, 2016
Kagera Sugar Vs Mtibwa Sugar
Machi 19, 2016
Coastal Union Vs Simba SC
Azam FC Vs JKT Ruvu
Majimaji Vs Mbeya City
Stand United Vs Ndanda FC
Machi 20, 2016
African Sports Vs Prisons
Machi 21, 2016
Mgambo JKT Vs Toto Africans
Machi 22, 2016
Mtibwa Sugar Vs Azam FC
Machi 23, 2016
Yanga SC Vs Mwadui FC
Machi 24, 2016
African Sports Vs Toto Africans

LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja tu, African Sports wakiikaribisha Mbeya City Uwanja wa Mkwakwani, Tanga katika vita ya kuepuka kushuka daraja.
African Sports inashika mkia katika Ligi Kuu ya timu 16, baada ya kuambulia pointi 17 tu katika mechi 22 ilizocheza hadi sasa, wakati Mbeya City ni ya tisa ikiwa na pointi 24 za mechi 22, ambazo bado haziwahakikishii kubaki Ligi Kuu.
Maana yake, Mbeya City inayofundishwa na kocha Mmalawi, Kinnah Phiri itahitaji ushindi leo ili kuendelea kujiondoa kwenye maeneo ya hatari.
African Sports ya kocha Aluko Ramadhani wazi ikiwa katika msimu wake wa kwanza tangu ipande Ligi Kuu – inapambana kutafuta nafasi ya kubaki kwenye michuano hiyo msimu ujao.
Ligi Kuu itaendelea keshokutwa kwa mchezo mmoja pia, kati ya Azam FC na Stand United Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Kwa Stand United ikiwa na pointi 30 baada ya kucheza mechi 22 haina nafasi ya ubingwa na wala haimo kwenye hatari ya kushuka daraja, hivyo huo ni mchezo ambao hauwatii ‘presha’ hata kidogo.
Lakini Azam FC ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi zake 47 za mechi 20 katika mbio za ubingwa dhidi ya Yanga yenye pointi 50 za mechi 21 na Simba iliyo kileleni kwa pointi zake 54 za mechi 23 – inahitaji ushindi ili kujiimarisha.  
Na baada ya kurejea Dar es Salaam jana kutoka Afrika Kusini ilikowachapa 3-0 wenyeji Bidvest Wist katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC imeingia kambini moja moja katika hosteli zake za Azam Complex, Chamazi kujiandaa na mchezo huo.
Mabingwa watetezi, Yanga wao watarudi kwenye Ligi Kuu baada ya mchezo wao wa marudiano wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya APR ya Rwanda Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga walioifunga APR 2-1 katika mchezo wa kwanza Jumamosi mjini Kigali – waterejea kwenye Ligi Kuu Machi 23, wakiikaribisha Mwadui FC Uwanja wa Taifa.
Simba itaendelea kukimbizwa katika Ratiba ya Ligi Kuu kwa kucheza na Coastal Union Jumamosi Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger