Habari niliyoipokea muda mfupi uliopita zinamhusu Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof Jumanne Magembe kumsimamisha kazi Mkurugenzi msimamizi wa wanyama pori Charles Mulokozi
kwa kutoa vibali vya kusafirisha wanyama kwenda nje pamoja na
wakurugenzi wanne wa Huduma za misitu kutokana na usafirishaji na
uvunaji holela wa magogo.
Akizungumza na kituo cha ITV Waziri Magembe amesema….>>>‘watu
wanavuna mazao ya misitu kule kalambo, tukaenda kule tukakutana na
magogo mengi sana yako msituni ambayo yanatakiwa yawe yamelipiwa na
hayakulipiwa, nimewaondoa hili tuweke uongozi mpya kwa sababu kinachoonekana ni kwamba hawana uwezo wa kuongoza’
Kuhusu kumsimamisha kazi Mkurugenzi msimamizi wa wanyama pori Charles Mulokozi, Waziri Magembe amesema .…..>>>Jana
usiku tumekamata ndege ambayo ilikuwa inasafirisha nyani, inaonekana ni
biashara inayofanywa kwa hiyo amesimamishwa kazi, uchunguzi ufanywe ili
tuone hili jambo la kusafirisha wanyama nje ya nchi limefanywa kiasi
gani na ni nani anafanya’
0 comments:
Post a Comment