Mmiliki
wa klabu wa Chelsea, Roman Abramovich ameudhibitishia uongozi wa Chelsea
na wachezaji wa klabu hiyo kuwa kocha Antonie Conte ndiyo ataiongoza
klabu hiyo baada ya msimu huu kumalizka.
Mtandao
wa Express Sport umeripoti kuwa Conte alikutana na Abramovich kuzungumza
kuhusu dili hilo la kuiongoza Chelsea kwa mkataba wa miaka mitatu ukiwa
na thamani ya Pauni Miloni 18.
Hatua
hiyo ya kumchukua Conte kuwa kocha wa Chelsea limekuja baada ya kocha
huyo wa Italia kutangaza kuachana na kazi ya kuiongoza Italia baada ya
kumalizika kwa mashindano ya Euro 2016 ambayo yatafanyika Ufaransa mwezi
Juni na Julai mwaka huu.(P.T)
0 comments:
Post a Comment