Mkutano
Mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliokuwa
ufanyike mwezi Disemba mwaka jana sasa utafanyika wikiendi hii Jumamosi
na Jumapili tar 12-13 March 2016 jijini Tanga.
Ajenda za mkutano huu ni kwa mujibu wa katiba ya TFF. Mkutano mkuu
utahitimishwa kwa uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha kukuza na
kuendeleza vipaji vya uchezaji mpira, kituo kitakachojengwa jijini
Tanga.
Mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa hoteli ya Regal Naivera.
0 comments:
Post a Comment