Sepp Blatter ameliongoza Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) kwa kipindi cha miaka 17.
Sepp
Blatter, raia wa Uswisi, ambaye alichaguliwa kwa muhula wa tano Mei 29
kuliongoza Shirikisho la Soka Duniani Fifa, ametangaza katika mkutano na
waandishi wa habari Jumanne Mei 2 katika mji wa Zurich kwamba
amejiuzulu kwenye wadhifa wake.
Uamzi huu unakuja kufuatia kashfa ya rushwa inayolikabili Shirikisho la Soka Dunia Fifa tangu Mei 27.
Akiwa ni
mwenyekiti wa Fifa tangu mwaka 1998, Sepp Blatter ametangaza kujiuzulu
Jumanne wiki hii katika mji wa Zurich, siku tano baada ya kuchaguliwa
kwa muhula wa tano kama mwenyekiti wa Shirikisho hilo la kandanda
Duniani.(P.T)
“ Nataka
kuitisha mkutano wa dharura na kukabidhi muhula wangu kwa yoyote yule
atakayeshinda katika kinyanga'nyiro cha kuwania nafasi ya mwenyekiti wa
Fifa”, amesema Blatter.
Sepp
Blatter na timu yake wanatuhumiwa kutoa kiholela masoko ya maandalizi ya
michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi na Kombe la Dunia
mwaka 2022 nchini Qatar.
“ Hata
kama nilichaguliwa, sikupata uungwaji mkono wa pande zote ”, amesema
Blatter katika mkutano na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya
Fifa.
Sepp
Blatter, mwenye umri wa miaka 79, amekua akishikilia wadhifa huo tangu
mwaka 1998. Mswisi huyo amebaini kwamba ataitisha mkutano wa dharura
kati ya mwezi Desemba mwaka 2015 na Machi mwaka 2016.
“
Ntaendelea kushikilia wadhifa wangu kwa muda wa miezi kadhaa, kabla ya
kumkabidhi mwenyekiti mpya atakaye kuwa amechaguliwa", ameongeza Joseph
Sepp Blatter.
Ni uamzi mzuri, kwa mujibu wa Michel Platini
Rais wa
Shirikisho la Soka barani Ulaya (Uefa), Michel Platini, amekaribisha
uamzi huo wa Sepp Blatter. Lakini baadhi ya marais wa mashirikisho ya
Soka kutoka mataifa ya Afrika wameshtushwa na uamzi huo, hasa Constant
Omari, rais wa shirikisho la Soka la Congo, ambaye amemsifu Sepp Blatter
kuwa ni mtu jasiri na mwenye uamzi.
Na RFI
0 comments:
Post a Comment