Fowadi wa Barcelona Gerard Deulofeu
Everton wamemsaini Fowadi wa Barcelona Gerard Deulofeu kwa Dau la Pauni Milioni 4.3.
Deulofeu, mwenye Miaka 21 na ambae ameichezea Spain mara 1, alikuwa
na Everton kwa Mkopo Msimu wa 2013/14 na kisha kurejea Barcelona ambapo
Msimu uliopita alipelekwa tena nje kwa Mkopo safari hii huko Sevilla.
Mchezaji huyo ataanza kuwa Mchezaji rasmi wa Everton kuanzia Julai 1 na amesaini Mkataba wa Miaka Mitatu.
Bosi wa Everton, Roberto Martinez, amesema anaamini Deulofeu ana nafasi ya kukuwa na kuwa Mchezaji bora zaidi.
Deulofeu anakuwa Mchezaji wa Pili kusainiwa na Everton katika
kipindi hiki baada ya kumpata Kiungo wa England Tom Cleverley aliejiunga
kama Mchezaji Huru baada ya Mkataba wake na Manchester United
kumalizika kufuatia kuichezea Aston Villa kwa Mkopo Msimu uliopita.
0 comments:
Post a Comment