Home » » EVERTON YASAJIRI FORWARD WA BARCELONA

EVERTON YASAJIRI FORWARD WA BARCELONA

 
Fowadi wa Barcelona Gerard Deulofeu 
Everton wamemsaini Fowadi wa Barcelona Gerard Deulofeu kwa Dau la Pauni Milioni 4.3.
Deulofeu, mwenye Miaka 21 na ambae ameichezea Spain mara 1, alikuwa na Everton kwa Mkopo Msimu wa 2013/14 na kisha kurejea Barcelona ambapo Msimu uliopita alipelekwa tena nje kwa Mkopo safari hii huko Sevilla.
Mchezaji huyo ataanza kuwa Mchezaji rasmi wa Everton kuanzia Julai 1 na amesaini Mkataba wa Miaka Mitatu.
Bosi wa Everton, Roberto Martinez, amesema anaamini  Deulofeu ana nafasi ya kukuwa na kuwa Mchezaji bora zaidi.
Deulofeu anakuwa Mchezaji wa Pili kusainiwa na Everton katika kipindi hiki baada ya kumpata Kiungo wa England Tom Cleverley aliejiunga kama Mchezaji Huru baada ya Mkataba wake na Manchester United kumalizika kufuatia kuichezea Aston Villa kwa Mkopo Msimu uliopita.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger