Home » » SUMAYE ASISITIZA KUHAMA CCM

SUMAYE ASISITIZA KUHAMA CCM


Mawaziri Wakuu Wastaafu, Fredrick Sumaye (kulia) na Edward Lowassa wakifurahia jambo
Mawaziri Wakuu Wastaafu, Fredrick Sumaye (kulia) na Edward Lowassa wakifurahia jambo
 
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, amekitahadhalisha Chama cha Mapinduzi (CCM), kuacha kuteua mgombea Urais, ambae anatumia fedha kuwahonga wananchi ili wamchague katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba.  
Sumaye amesema endapo chama chake kitamteua mgombea urais ambae ni mtoa rushwa na muabudu rushwa, atakihama chama hicho na kwamba hatakubali kuona jina lake linakatwa kirahisi na akaendelea kuvumilia.
Sumaye ametoa kauli hiyo  wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Shinyanga, ambamo amesema endapo atakatwa jina lake kiharari na mgombea kuteuliwa  ambae sio muabudu rushwa atakuwa tayari kusaidiana nae.
Amesema kuwa baadhi ya wagombea waliotangaza kuwania urais kupitia chama hicho, wengine kanuni haziwakubalibali bali wanasindikiza wenzao katika kinyang`anyiro hicho hivyo ana imani ataibuka kidedea.
“Watia nia 34 waliotangaza mpaka sasa, wapo wengine ambao hawaitaji urais na wala kanuni za chama chetu haziwakubali hao wanasindikiza wenzao, hao tayari wameishajitoa wenyewe na siwafikirii”.amesisitiza Sumaye
Hata hivyo amesema chama hicho kinapaswa  kuteua mtu ambae ni msafi asiekuwa na kashfa yeyote atakaesababisha chama hicho kushindwa kutwaa dola katika uchaguzi mkuu wa Oktoba Mwaka huu.
Amesema umefika wakati wa CCM kutafakari na kuchuja watangaza nia waliojitokeza hata wale ambao wanasindikiza wenzao katika safari hiyo, ili kutoa mtu ambaeambae ana nia thabiti kuwatumikia wananchi.
Ameongeza  uchaguzi huu  utakuwa na vitimbwi na vituko vya kila aina hivyo watanzania wanapaswa kuwa watulivu katika kufanikisha kumpata kiongozi ambae ni bora na muadilifu.
Amesema vyama vya siasa nchini vinapaswa kutoa maelekezo mazuri kwa wananchama na wafuasi wao ili kuepusha vurugu zisizokuwa za lazima katika uchaguzi huo na nkutetea maslahi ya umma.
“Siasa ni hoja na wala siasa sio kutumia nguvu, nondo, risasi, rungu na panga ili kuingia ikulu, hapana ni kutumia hoja nzuri na kuwaelimisha wafuasi katika kufanya mambo ambayo ni mazuri,” amesema  Waziri huyo wa zamani.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger