Home » » CHADEMA WATAWANYWA KWA MABOMU IRAMBA,MKOANI SINGIDA

CHADEMA WATAWANYWA KWA MABOMU IRAMBA,MKOANI SINGIDA



Polisi yawatawanyisha CHADEMA kwa mabomu..

    Jeshi la polisi wilayani Iramba limetumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya wanachama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kuwakamata Mwenyekiti wa uhamashishaji kanda ya kati Bi Jesca Kishoa na katibu wa BAVITA wilayani Iramba Bwana Rayman Minja, wakati walipokuwa wakiwahamasisha wananchi kwenye mkutano wa hadhara kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. ,
    Akieleza baada ya kuachiwa na jeshi la polisi alipokuwa amewekwa chini ya usalama kwa zaidi ya masaa matano mwenyekiti wa uhamashishaji CHADEMA kanda ya kati Bi. Jesca Kishoa, amesema anashangaa kuona Mkuu wa Wilaya ya Iramba akiwakataza kufanya mikutano huku vyama vingine vimekuwa vikifanya mikutano, jambo ambalo hastahili kufanya hivyo kwa sababu yeye anatawala wananchi wenye vyama tofauti na siyo chama kimoja.
    Kwa upande wao, wananchi wa wilaya ya Iramba wametupia lawama kwa jeshi la polisi kuzuia mikutano minne ya CHADEMA, pia kutumia nguvu kutawanya watu kwa kuwa mwagia maji ya kuwasha na kuwapiga mbomu ya machozi.
    Akionge kwa simu kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida, Bwana Thobias Sedoyeka amesema wao wanatekeleza amri ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba ya kupiga marufuku na kuzuia mikutano yoyote ya hadhara ifanyike wilayani humo.
    Taarifa via ITV
    Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

    0 comments:

     
    Supported by AMAGA Media services : | |
    Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
    Templete Designed by Abdallah Magana
    Proudly powered by Blogger