Home » » POLISI WATUMIA MABOMU YA MACHOZI KUWATAWANYA WANAFUNZI WA CHUO CHA KAMPALA

POLISI WATUMIA MABOMU YA MACHOZI KUWATAWANYA WANAFUNZI WA CHUO CHA KAMPALA

 
Polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia FFU wametumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya wanafuzi wa chuo kikuu cha kampala kilichopo Gongo la mboto jijini Dar es Salaam baada ya kufanya mgomo kwa ajili ya kushinikiza kupatiwa majibu juu ya usajili wa kozi ya Famasia.
Kabla ya polisi kuchukuwa hatua hiyo wanafunzi hao walifanya maandamano ndani ya chuo hicho huku wakiimba nyimbo mbalimbali za mashinikizo na wakiweka kambi nje ya jengo la utawala hali iliyosababisha uongozi wa chuo kufunga chuo kwa muda usiojulikana na kuwataka waondoke bila mafanikio.
 
Hata hivyo baada ya muda mfupi magari ya polisi yaliongezeka yakiwa na polisi waliokuwa na mabomu ya machozi na silaha za moto na baadae gari la maji ya kuwasha likawasili na hapo ndipo vurugu zikaanza wakati polisi wanawamwagia maji ya kuwasha wakaanza kurusha mawe, mabomu ya machozi yakafuatia hali iliyopelekea wanafunzi kadhaa kujeruhiwa na wengine kukamatwa na polisi.
 
Mara baada ya sakata hilo kiongozi wa wanafunzi wanaosoma kozi ya famasia Bw.Levid Pavela akazungumza na waandishi wa habari ambapo amesema mgomo huo ni mara ya tatu na ulitokana na baadhi ya wanafunzi waliohitimu kozi hiyo kushindwa kuajiriwa kwa madai haitambuliki na bodi ya famasia huku akizungumzia tukio hilo.
 
Akizungumzia suala hilo naibu mkurugenzi wa kitengo cha udahili wa chuo hicho Bw. Lotha Samora amekiri kuwa bado hawajapata usajili wa kozi hiyo na kuongeza kuwa walishapeleka maombi bodi ya Famasia tangu mwaka 2011 lakini hadi leo hawajafanikiwa.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger