Home » » PAUL NONGA AMFUATA JULIO.....AJIFUNGA MWAKA MMOJA MWADUI FC

PAUL NONGA AMFUATA JULIO.....AJIFUNGA MWAKA MMOJA MWADUI FC

      

 

Klabu ya Mwadui ya mkoani Shinyanga imefanikiwa kumsajili mshambuliaji Paul Nonga kutoka katika klabu ya Mbeya City kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Nonga ametua katika klabu hiyo iliyopanda daraja msimu huu kufuatia mkataba wake katika klabu ya Mbeya City kumalizika.

Akiongea na Ukurasa Wa Habari kutokea moja kwa moja mkoani Shinyanga mchana huu, Nonga amesema kikubwa zaidi ni kutafuta changamoto mpya na upande wa masirahi pia mwadui wapo vizuri. "Mimi nimefurahi kurudi nyumbani ,hii ni changamoto mpya na kingine kilichonishawishi kuja hapa ni masuala ya masirahi ,mwadui wapo vizuri "amesema Nonga

Mshambuliaji huyo ni moja ya wachezaji waanzilishi wa Mwadui Fc,aliichezea timu hiyo miaka ya nyuma wakati wanatafuta nafasi ya kupanda ligi daraja la kwanza lakini wakashindwa baada ya Rhino Rangers kuwapiku.

Baada ya hapo Nonga alihamia jkt Oljoro na baadaye Mbeya City ambapo amecheza kwa misimu miwili huku akiwa mshambuliaji tegemezi wa timu hiyo ya jijini Mbeya

Mwadui iliyopo chini ya kocha mwenye maneno mengi Jamhuri Julio Kihwelu itacheza katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu ujao mara baada ya kufanikiwa kupanda daraja msimu huu kuingia kunako ligi hiyo.

                                                         
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger