Home » » "PANYA ROAD" WATINGISHA TABATA

"PANYA ROAD" WATINGISHA TABATA

Baadhi ya Panya Road waliowahi kukamatwa
Baadhi ya Panya Road waliowahi kukamatwa
KUNDI la vijana waporaji maarufu kama “Panya Road” linadaiwa kuvamia eneo la Tabata jijini Dar es Salaam na kuwashambuli watu kwa mapanga na nondo kisha kuwapora fedha na simu katika mitaa ya Kimanga na Kisukuru.  
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Wilaya ya Ilala, Lucas Mkondya, alipotakiwa  kuthibitisha tukio hilo, alikiri kuwa na taarifa hizo lakini akasema hawezi kuzungumza na mwandishi kwenye simu.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, hakuweza kupatikana katika simu yake ya kiganjani.
Kwa mujibu wa walioshuhudia tukio hilo, amesema lilitokea saa 11 jioni jana ambapo wananchi waliporwa mali zao kabla ya askari polisi waliokuwa doria kuzima tukio hilo.
“Hilo kundi lilikuwa vijana wengi wametusumbua sana maeneo ya Tabata na kuwapora watu vitu vyao, ukiwa mbishi unakatwa mapanga,”amesema shuhuda huyo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, “Panya Road” hao walikuwa wakilipiza kisasi baada ya mwenzao kuuliwa na wananchi wenye hasira baada ya kumuibia mteja simu katika klabu moja maarufu iliyoko maeneo ya Tabata.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger