Copa America, Kombe la Mataifa ya Marekani ya Kusini, linaanza Nchini Chile Wikiendi ijayo na Nchi hizo zipo kwenye matayarisho makali huku Mabingwa Watetezi Uruguay wakiiadhibu Guatemala 5-1 na Argentina kuwawasha Bolivia 5-0
Uruguay, wakicheza bila ya Luis Suarez ambae yuko Kifungoni na pia
alikuwa huko Berlin kuichezea Barcelona kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONZ
LIGI, waliichapa Guatemala Bao 5-1 kwa Bao za Diego Rolan, Edinson
Cavani, Bao 2, Giorgian De Arrascaeta na Abel Hernandez.
Uruguay watafungua utetezi wa Taji lao la Copa America huko Nchini
Chile kwa kucheza na Jamaica Juni 13 na kisha kucheza na Argentina na
Paraguay katika Mechi za Kundi B.
Hata hivyo, Uruguay hawawezi kumtumia Luis Suarez ambae anatumikia
Kifungo cha Mechi 9 kwa kumng'ata Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini
Mwaka Jana kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.
Nao Argentina, wakicheza bila ya Lionel Messi, Javier Mascherano na
Carlos Tevez, ambao walikuwa wakichezea Klabu zao kwenye Fainali ya
UEFA CHAMPIONZ LIGI wakati Barcelona wakicheza na Juventus huko Berlin,
waliinyuka Bolivia Bao 5-0 huko Estadio San Juan del Bicentenario Mjini
San Juan.
Bao za Argentina zilipigwa na Sergio Aguero, Bao 3, na Angel Di Maria Bao 2.
Nako huko Diego Armando Maradona Stadium Mjini Buenos Aires Nchini
Argentina, Radamel Falcao alifunga Bao la ushindi wakati Colombia
inaitungua 1-0 Costa Rica.
0 comments:
Post a Comment