Home » » VAN GAAL KUMTAMBULISHA DEPAY LEO.

VAN GAAL KUMTAMBULISHA DEPAY LEO.


LVG-GIGGS-MAKOCHA                                                                                                                                                                   Meneja wa Manchester United Louis van Gaal Leo, kwa mara ya kwanza tangu Timu ikusanyike kwa ajili ya Mazoezi kwa Msimu mpya, ataongea na Wanahabari huko Jijini Manchester.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi, Van Gaal pia atamtambulisha rasmi Mchezaji mpya wao, Memphis Depay, waliemnunua Mwezi uliopita kutoka PSV Eindhoven ya Holland.
Huku kukiwa na habari tele za Man United kumnasa Beki wa Kimataifa wa Italy, Matteo Darmian, anaechezea Torino, ambae Leo anasemekana atapimwa Afya yake, na pia kuuzwa kwa Robin van Persie kwa Fenerbahce na Angel Di Maria kwa PSG, Wadau wa Man United wana shauku kubwa kujua Van Gaal atatoboa kipi zaidi.
Shauku hiyo pia inakolezwa na zile habari za kila Siku za Man United kuhusishwa na kununua Wachezaji wapya wakitajwa sana Mastaa kama Nicolas Gaitan, Nicolas Otamendi, Morgan Scneiderlin na lukuki kadhaa wengine.
Man United inatarajiwa kuruka kwenda Marekani Jumatatu Julai 13 kuanza Ziara yao na pia kutetea Taji lao la International Champions Cup walilotwaa Mwaka Jana huko huko USA.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger