Home » » PICHA:: Taarifa za kuvamiwa kwa kituo cha Polisi STAKISHARI Jijini Dar

PICHA:: Taarifa za kuvamiwa kwa kituo cha Polisi STAKISHARI Jijini Dar

 

 

 Watu waliokisiwa kuwa majambazi wamekivamia kituo cha polisi Stakishari ukonga.  Kwa mujibu wa taarifa za awali watu hao inasemekanaya wamevunja store ya  silaha na kuchukua silaha zote aina ya SMG zilizopo kituoni hapo….hadi sasa inasemekana kuna vifo vya polisi  ambao idadi yake haijajulikana wameuwawa  na pia kuna  jambazi mmoja aliyepigwa na risasi ya jambazi mwenzie….Jambazi huyo aliyeuwawa inasemekana ni dereva wa bodaboda wa kituo cha Nji Panda aliyefahamika kwa jina la Madevu.

Taarifa hizo zinasema  majambazi hayo yametokomea na kuacha pikipiki 3….hali si shwari mitaa ya Stakishari na maeneo ya karibu baada ya milio ya bunduki kutawala maeneo yote. watu walio wengi wamejifungia majumbani mwao na sasa hivi kelele za  ving’ola  vya magari ya polisi vinasikika Stakishari maeneo yote……kwa habari zaidi tuendelee kufuatilia

Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger