Home » » BENITEZ: RAMOS ANABAKI SANTIAGO BERNABEU!

BENITEZ: RAMOS ANABAKI SANTIAGO BERNABEU!

SERGIO-RAMOS

                                                                                                                                                                                  Meneja mpya wa Real Madrid Rafael Benitez ametoboa kuwa Beki wao Sergio Ramos hatahama.
Mwezi Juni Manchester United ilitoa Ofa ya Pauni Milioni 28.6 kumnunua Beki huyo wa Kimataifa wa Spain na Ofa hiyo kugomewa na Real.
Hivi sasa Man United wanaisuka upya Timu yao chini ya Meneja Louis van Gaal na tayari wameshanunua Wachezaji wapya Wanne, ambao ni Viungo Bastian Schweinsteiger na Morgan Schneiderlin, Fulbeki wa Kulia Matteo Darmian na Winga Memphis Depay, huku Robin van Persie na Nani wakiiuzwa kwa Klabu ya Uturuki Fenerbahce.
Ilitarajiwa Sergio Ramos atatua Man United huku Kipa wao David De Gea akienda Real lakini inaelekea Dili hii imekwama huku kila upande uking'ang'ania matakwa yake.
Lakini Wachambuzi wengi walikuwa na imani kuwa nia halisi ya Ramos si kuhama Real bali kuishinikiza Klabu hiyo iboreshe Mkataba wake.
Nao Man United hawana nia yeyote ya kumuuza David De Gea na wako tayari kukaa nae hadi mwishoni mwa Msimu ujao ambapo Mkataba wake utakapoisha na aondoke bure tu.
Hata hivyo zipo pia habari kuwa ikiwa De Gea ataondoka hivi sasa basi Man United inataka ilipwe si chini ya Pauni Milioni 33 ili kumfanya Kipa huyo awe wa Bei ghali katika Historia na kupiku Dau ambalo Juventus lilitoa kumnunua Kipa wao Gianluigi Buffon kutoka Parma Mwaka 2001 walipolipa Pauni Milioni 32.1
Akiongea kuhusu Ramos, ambae Real wamesafiri nae kwenye Ziara yao huko Australia, Benitez amesema: "Mengi yamezungumzwa kuhusu Ramos. Kwangu mimi Rais ashatamka anabakia Real. Namuona Ramos kama sehemu muhimu ya mipango yetu hapa Real. Yeye ni mshindi na hilo ndio tunataka kwa Timu yetu. "
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger