Home » » BASTIAN SCHWEINSTEIGER KUJIUNGA RASMI NA MAN UNITED!

BASTIAN SCHWEINSTEIGER KUJIUNGA RASMI NA MAN UNITED!

 
schweini                                                                                                                                                        MTENDAJI MKUU wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge, ametangaza kuwa wamekubaliana na Manchester United kuhusu kumuuza Nahodha wa Germany, Bastian Schweinsteiger taarifa ambazo pia zimethibitishwa huko Old Trafford kupitia Tamko rasmi kwenye Tovuti yao. 
Schweinsteiger, mwenye Miaka 30, alikuwa pamoja na Meneja wa Man United Louis van Gaal huko Bayern kati ya Miaka 2009 na 2011 wakati Van Gaal alipokuwa Meneja na wana uhusiano mzuri sana.
Kauli hii ya Rummenigge inadhihirisha makubaliano ya pande hizo mbili kuhusu Ada ya Uhamisho ambayo inasemekana ni Pauni Milioni 6.
Mapema hii Leo, Gazeti kubwa huko Germany, Bild, liliripoti kuwa Schweinsteiger atasaini Mkataba wa Miaka Mitatu na Man United utakaomlipa Pauni 140,000 kwa Wiki, ikiwa ni ongezeko kubwa kupita Bayern, na alikuwa akisubiri kuruka kwenda Jijini Manchester kupimwa Afya pindi tu Klabu hizo zikiafikiana Ada yake ya Uhamisho.
Gwiji huyo wa Germany alikuwa amebakiza Mwaka mmoja tu kwenye Mkataba wake na Bayern.
Kufuatia uthibitisho huu, Schweinsteiger, akifuzu upimwaji Afya na taratibu nyingine, atakuwa Mchezaji wa 3 kutua Man United baada ya Memphis Depay na Matteo Darmian ambae nae pia yuko hatua za mwisho kukamilisha Uhamisho wake kutoka Torino ya Italy.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger