Home » » ARDA TURAN HATUA RASMI BARCELONA

ARDA TURAN HATUA RASMI BARCELONA

TURAN-BARCA
 
 Barcelona imemsaini Nahodha wa Turkey, Arda Turan, kwa Mkataba wa Miaka Mitano kutoka Atlético Madrid kwa Dau la awali la Pauni Milioni 24.1.
Kiungo huyo mwenye Miaka 28 amekuwa akiandamwa na Klabu kubwa huko Ulaya, ikiwemo Chelsea, baada ya kutobolewa anataka kuihama Atletico.
Dili ya kumnunua Turan imegubikwa na utata kwani hivi sasa Barcelona ipo kwenye Uchaguzi wa Rais wake na hivyo inaendeshwa na Kamisheni maalum hadi atakapopatikana Rais mpya na ilibidi Kamisheni hiyo ndio ipitishe uamuzi wa kumsaini Turan.
Lakini pia Dili hii ina Kipengele cha ajabu kwenye Mkataba wa Turan ambacho kinatamka yeyote atakaeshinda Urais wa Barcelona kwenye Uchaguzi hapo Julai 18 anaweza, ndani ya Siku 2 tokea hapo, kumuuza tena Turan kwa Atletico kwa Dau la pungufu ya Asilimia 10 ya Ada ya Uhamisho iliyolipwa.
Hata hivyo, kutokana na Adhabu ya FIFA ya kuifungia Barcelona kutonunua Wachezaji hadi Mwakani, Turan hawezi kuichezea Barcelona hadi Januari 2016.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger