Home » » AL-SHABAAB WAUA WATU 14 NCHINI KENYA

AL-SHABAAB WAUA WATU 14 NCHINI KENYA

 

Maofisa wa polisi wakiwa eneo la tukio lilipotokea shambulio lililoua watu 14 usiku wa kuamkia leo.
Takribani watu 14 wameuawa, 11 wakijeruhiwa baada ya Al-Shabaab kushambulia kijiji cha Soko Mbuzi kilichopo jirani na Mji wa Mandera nchini Kenya usiku wa kuamkia leo. Mamlaka husika huko Mandera yathibitisha.
Mashuhuda wa tukio hilo wameeleza kuwa shambulio lilitokea saa 7 usiku wa kuamkia leo wakati wakazi wa Kijiji cha Soko Mbuzi wakiwa wamelala.
Shambulio hilo limeelezwa kuwalenga wafanyakazi wa machimboni ambao wengi wao siyo wenyeji.

Taswira kutoka Kijiji cha Soko Mbuzi lilipotokea shambulio.

Wananchi wakiwa eneo hilo la tukio.
(Picha zote na Daily Nation)
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger