Home » » RVP KUUUNGANA NA NANI FENERBAHCE

RVP KUUUNGANA NA NANI FENERBAHCE

RVP-EVANS                                                                                                                                                                                                                                Manchester United wako njiani kumpa mkono Straika wao Robin van Persie ambae tayari kuna makubaliano ahamie Uturuki Klabuni Fenerbahce.
RVP
Tayari Fenerbahce ishakubaliana Mkataba wa Miaka Minne na Robin van Persie ili ahamie hapo kutoka Manchester United.
Hivi karibuni, Mkurugenzi wa Fenerbahce, Guiliano Terraneo, alitua huko England kukamilisha Dili hiyo na Van Persie, Raia wa Netherlands mwenye Miaka 31, ambae Mkataba wake wa sasa na Man United umebakiza Mwaka mmoja tu.
Ikiwa Dili hii itakamilika, basi Van Persie ataungana huko Uturuki na Mchezaji mwingine aliekuwa Man United, Nani, ambae Siku mbili zilizopita alihamia Fenerbahce kwa Dau la Pauni Milioni 4.5.
Lakini kuhama kwa Robin van Persie kutaifanya Man United ibaki na Mafowadi wanaotambulika Wawili tu, Kepteni Wayne Rooney na Chipukizi James Wilson.
Fowadi wao mwingine aliebaki ni Javier Hernandez 'Chicharito' ambae Msimu uliopita alitupwa kwa Mkopo huko Real Madrid na sasa anapaswa kurudi Old Trafford lakini Wiki iliyopita alivunjika Mfupa wa Begani na kufanyiwa Operesheni itakayomweka nje kwa takriban Miezi Miwili.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger