Home » » FABIO CAPELLO ATIMULIWA URUSI!

FABIO CAPELLO ATIMULIWA URUSI!


fabio-capello-pic-getty-843858221                                                                                                                                                                    Fabio Capello ameondolewa kama Kocha Mkuu wa Russia baada kushika wadhifa huo kwa Miaka Mitatu.
Mwaka Jana, Capello alisaini nyongeza ya Mkataba wake kwa Miaka Minne ambao ungemweka huko Urusi hadi baada ya Fainali za Kombe la Dunia za    Mwaka 2018 ambazo Urusi ndio Wenyaji wake.
Lakini, baada ya matokeo mabovu, ambayo yameifanya Russia iwe na Pointi 8 tu katika Mechi 6 za kufuzu Fainali za EURO 2016, Russia imestuka.
Hata huko Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia Mwaka Jana Russia, chini ya Capello, ilitupwa nje hatua za Makundi tu bila ya kushinda hata Mechi moja katika Mechi zao 3.
Chama cha Soka cha Russia (RFU kimesema kimefikia makubaliano na Kocha huyo kutoka Italy, ambae pia aliwahi kuifundisha England, kuutengua Mkataba wake.
Inaaminika RFU imemlipa Capello Euro Milioni 15 kufuatia uamuzi huo.
Mwezi uliopita, Mashabiki wa Russia walianzisha kampeni ya kuchangishana Fedha ili kuununua Mkataba wa Capello na kumng'oa.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger