Home » » LIVERPOOL YAMTEMA STERLING, CITY YAPANDISHA DAU KUMNUNUA!

LIVERPOOL YAMTEMA STERLING, CITY YAPANDISHA DAU KUMNUNUA!

 
raheem-sterling 2                                                                                                                                                           Liverpool imeamua kutomchukua Winga wao Raheem Sterling kwenye Ziara yao ya huko Mashariki ya Mbali na Australia ambayo Leo hii wanapaswa kusafiri wakati Manchester City ikipandisha Dau lao la kumnunua na kufikia Pauni Milioni 45.
Awali Man City ilitoa Ofa mbili, zote zikikataliwa, na ya mwisho ilikuwa ni Pauni Milioni 40 wakati Liverpool wanamthamini Mchezaji huyo kuwa ni Pauni Milioni 50.
Ripoti toka huko England zinadaia Mchezaji huyo ameachwa kwenye Ziara ili akamilishe Uhamisho huu kwenda City baada ya Majuzi kutoonekana Mazoezini kwa Siku 2 akidai Mgonjwa na Ijumaa kuibuka tena Mazoezini.
Sakata la Sterling na Liverpool lilianzia Januari alipogomea Mkataba mpya ambao ungemlipa Mshahara kwa Wiki wa Pauni 100,000 toka 35,000 za sasa.
Baada ya hapo, Wakala wa Sterling, Aidy Ward, akachochea zaidi kwa kudai Sterling hatasaini Mkataba wowote mpya hata akilipwa Pauni Laki 9 kwa Wiki kitu ambacho Liverpool kiliwaudhi sana na kumsusia Wakala huyo.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger