Home » » EUROPA LIGI: LEO MECHI 51 KUPIGWA, WEST HAM YASAKA KUTINGA RAUNDI YA PILI!

EUROPA LIGI: LEO MECHI 51 KUPIGWA, WEST HAM YASAKA KUTINGA RAUNDI YA PILI!

EUROPALIGI-NICE-2                                                                                                                                                        Meneja mpya wa West Ham Slaven Bilic Leo atakuwa Benchi kwa mara ya kwanza wakati Timu yake ikicheza Mechi ya Marudiano ya Raundi ya Kwanza ya Mtoano ya EUROPA LIGI huko Nchini Andorra dhidi ya Lusitanos.
Katika Mechi ya kwanza iliyochezwa Upton Park Jijini London Wiki iliyopita, West Ham iliinyuka Lusitanos 3-0 huku Slaven Bilic akikaa Jukwaani na kumpisha Terry Westley, Kocha wa Vijana, kuongoza Timu.
Kitendo hicho cha Bilic kukaa Jukwaa la Watazamaji katika Mechi hiyo ya kwanza kilimkera mno Kocha wa Lusitanos, Xavi Roura, ambae alidai ni kuwavunjia heshima.
Kama ilivyo katika Mechi ya kwanza, hii Leo West Ham, ambao tayari wametangaza Wachezaji 11 watakaocheza, kitakuwa mchanganyiko wa Vijana na Maveterani wa Timu ya Kwanza wakiwemo Joey O'Brien, ambae hii itakuwa Mechi yake ya 100 kwa West Ham, na wengine ni James Tomkins, Morgan Amalfitano na Diafra Sakho, aliefunga Bao 2 katika Mechi ya kwanza.
Mmoja wa Vijana watakaocheza ni Lewis Page, mwenye Miaka 19, wakati Beki wa Miaka 16, Reece Oxford, akiwekwa Benchi.
Mbali ya Mechi hii ya West Ham na Lusitanos, pia Leo zipo Mechi nyingine za 50 za Marudiano za Raundi ya Kwanza ya Mtoano ya EUROPA LIGI.
KIKOSI CHA WEST HAM KITAKACHOANZA LEO: Randolph, O'Brien, Tomkins, Burke, Page, Amalfitano, Poyet, Cullen, Jarvis, Lee, Sakho. Subs: Spiegel, S Westley, Knoyle, Oxford, Nasha, Parfitt-Williams, Brown.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger