Kikosi
cha Simba jana Jumapili kimeendeleza moto wake wa kufanya vizuri katika
mechi zake baada ya kuitandika Nidham FC inayomilikwa na Jeshi la
Wananchi Tanzania (JWTZ) mabao 11-1.
Simba
inayofundishwa na Mganda, Jackson Mayanja, ilipambana na Nidhamu FC
katika mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi
jijini Dar es Salaam.
Mchezo
huo ulikuwa maalum kwa Simba ambayo hivi sasa ipo katika maandalizi
makali ya kujiandaa na mechi ya Kombe la FA dhidi ya Coasta Union ya
Tanga itakaopigwa Aprili 11, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam, lakini pia michuano ya Ligi Kuu Bara.
Mabao
ya Simba katika mechi hiyo yalifungwa na Said Ndemla aliyetupia mawili,
Awadhi Juma (2), Daniel Lyanga (2), Ibrahim Ajib (2) pamoja na Musa
Hassan ‘Mgosi’ (2) huku lingine likifungwa na kinda wa kikosi B cha timu
hiyo.
Kocha
Mkuu wa Simba, Jackson Mayanja ameliambia Championi Jumatatu kuwa,
pamoja na kikosi chake hicho kupata matokeo hayo bado kinatakiwa kiwe
bora zaidi ya hapo.
credit;Salehe Jembe
0 comments:
Post a Comment