Home » » Hakielimu yashauri bajeti ya Elimu 2016/2017

Hakielimu yashauri bajeti ya Elimu 2016/2017

Wanafunzi wakiwa katika shule iliyokuwa katika mazingira magumu
Wanafunzi wakiwa katika shule iliyokuwa katika mazingira magumu

  KATIKA kuelekea bunge la bajeti hivi karibuni, serikali imeshauriwa kuongeza bajeti ya sekta ya elimu kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ili kuendana na kauli ya upatikanaji wa elimu bure sambamba na kufidia gharama za uboreshaji na ujenzi wa miundombinu, 

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini hapa na John Kalage Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Hakielimu, wakati alipokuwa akitoa taarifa ya uchambuzi na ushauri wa Shirika la Hakieli juu ya mwelekeo wa bajeti ya elimu2016/2017.
Kalaghe amesema serikali haina budi kuongeza bajeti ya sekta ya elimu kwa mwaka wa fedha 2016/2017 hadi kufikia asilimia 20 ya bajeti ya taifa au asilimia 6 ya pato lote la taiafa.
Aidha amesema kwa mujibu wa uchambuzi walioufanya kama shirika, na kwa kuzingatia takwimu za idadi ya wanafunzi, shule na mahitaji, kila mwaka serikali itapaswa kutenga kiasi cha fedha kisichopungua Tsh. bilioni 1,034.5 nje ya mahitaji mengine ya kisekta ili kugharamia elimu bila malipo.
“Tunafahamu hivi karibuni bunge linatarajiwa kuanza vikao vyake na kama watetezi na mdau wa upatikanaji wa elimu bora nchini, tunapendekeza kwa serikali maeneo ambayo yanahitaji kutiliwa mkazo katika upangaji wa bajeti ya sekta ya elimu yazingatiwe” amesema Kalage.
Akizungumzia maeneo muhimu ambayo serikali inatakiwa kuyazingatia katika upangaji wake wa bajeti kupitia sekta hiyo amesema ni pamoja na eneo la bajeti ya utekelezaji wa elimu bila ada, upangaji wa bajeti ya sekta ya elimu, bajeti ya ukaguzi na uhakiki wa ubora wa elimu, mwongozo wa sera ya mpya ya elimu na makadirio bajeti ya sekta ya elimu 2016/2017.
Amebainisha kuwa eneo la bajeti ya utekelezaji wa elimu bila ada, linapaswa kuanza kutekelezwa kabla ya agizo la elimu bila ada, suala hilo lilikuwa likitekelezwa kupitia michango ya wazazi kwa kuchangia elimu kwa kushirikiana na serikali.
Aidha kuhusu gharama za kufidia ada na ruzuku shuleni kwaajili ya vifaa, gharama za mitihani na gharama za uendeshaji kwa shule za msingi na sekondari amesema, kwa kuwa gharama hizo zilikuwa zikifanikishwa awali kwa ushirikiano wa michango ya wazazi na serikali basi serikali inapaswa kufidia gharama zote kwa kutenga kiasi cha sh.bilioni 161.5 katika maeneo hayo.
Akielezea gharama za kufidia ujenzi na miundombinu ambao nao ulikuwa ukichangiwa na wazazi alisema serikali kufidia gharama hizo kwa kutenga bilioni 1, 438 huku kwa upande wa gharama za kufidia utoaji wa uji katika shule za msingi na awali itenge kiasi cha sh 198.
Vile vile kuhusu upangaji wa bajeti wa sekta ya elimu, ameshauri kuwa licha ya changamoto zilizopo katika upangaji wa matumizi katika sekta ya elimu, serikali inatakiwa kuangalia namna ya kuweka uwiano wa bajeti ya matumizi ya kawaida na ya maendeleo.
“Tunaona katika kipindi cha miaka mitano iliyopita wastani wa bajeti ya maendeleo ya sekta ya elimu imekuwa kati ya asilimia 11 hadi 16 tu wakati ile ya matumizi ya kawaida ikifikia asilimia 80 hadi 90, kihalali kiasi kinachotengwa ni kidogosana kulinganisha na changamoto,
“Mathalani bajeti ya mwaka 20215/2016 bajeti nzima ilikuwa sh. Bilioni 3,887 huku bajeti ya maendeleo ikiwa ni asilimia 16 tu” amesema.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger