Mashindano ya vilabu Kombe la Nile Basin huandaliwa na CECAFA kwa kushirikisha vilabu vilivyoshika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kwa nchi wanachama wa CECAFA.
Bingwa michuano ya kombe hilo atajinyakulia zawadi ya dola za kimarekani 30,000 (Zaidi ya milioni 60 za Tanzania), mshindi wa pili dola 20,000, huku mshindi wa tatu akipata kitita cha dola za kimarekani 10,000.
Nile Basin inashirikisha vilabu kutoka katika nchi wanachama wa CECAFA ambazo ni Burundi, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Sudan, Sudan Kusini, Tanzania na Zanzibar.
Vitoria University kutoka Uganda ndiyo mabingwa watetezi wa kombe hilo baada ya kuifunga AFC Leopards ya Kenya kwa mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliofanyika mwaka 2014.