Home » » Hivi ndivyo Fools’ Day ilivyotesa wa watu kwenye michezo.

Hivi ndivyo Fools’ Day ilivyotesa wa watu kwenye michezo.

 
cover
Leo April fools’ day watu wengi wamedanganywa na marafiki zao ikiwa ni moja ya sehemu ya kuadhimisha siku ya wajinga duniani. Sasa kwa upande wa soka nini kimetokea.
Haya ni baadhi ya matukio ambayo yametokea kwenye April fools day.
5
1)Southampton wametangaza logo mpya ambayo itatumika kwenye msimu ujao wa 2016/2017 ikiwa na kikatuni juu yake. Southampton walitangaza kupitia page zao za social networks nakusema kwamba wanajivunia kuwa club ambayo ipo mbele kwenye kufikiria na wanaamini logo mpya itawasaidia kupiga hatua mbele.
4
2)Arsenal nao wametangaza kwamba uwanja wao wa Emirates stadium utakua uwanja wa kwanza kuwa na paa linalojifunga full ili kuzuia jua. Arsenal wamesema cover hilo limetumia technolojia kwa msaada wa kampuni ua Citroen ya huko UK.
3
3)Rio Ferdinand alitangaza kwenye page yake ya twitter kwamba ame-sign mkataba wa kuwa manager mpya wa Manchester United. Hivyo basi anasubiri June ifike kwa hamu.
2
Lakini baada alijirudi na kusema kila mtu ana ndoto hiyo post ilikua ni kwa ajili ya fools’ day.
1
4)Bayern Munich waliandika Breaking news kwamba Zlatan ame-sign mkataba nao na wamempa jezi namba 10 mgongoni. IKumbukwe kwamba Zlatan yupo mbioni kuhama club hiyo.
Post zote hizi zilikua ni za uongo ikiwa ni njia ya kuadhimisha siku ya wajinga duniani.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger