Sheikh Ponda akiwa ndani ya Mahakama Kuu akisubiri hukumu.
Wakili wa Sheikh Ponda, Bw Juma Nassoro akizungumza jambo na mteja wake mahakamani hapo.
…. Nassoro akiteta jambo na Sheikh Ponda.
Askari akidumisha ulinzi mahakamani hapo.
Sheikh
Ponda akitoka nje ya Mahakama Kuu baada ya kushinda Kesi ya Ardhi
iliyokuwa ikimkabili kisha kurudi mahabusu katika gereza la Segerea.
….akipanda Karandinga la magereza.
Sheikh Ponda akiwa ndani ya gari la magereza tayari kwa kurudi rumande.
MAHAKAMA
Kuu ya Tanzania imemuachia huru aliyekuwa Katibu wa Taasisi za Kiislam,
Sheikh Ponda Issa Ponda baada ya kuona hana hatia dhidi ya Kesi ya
madai ya Ardhi ya Agrekanza inayomilikiwa na Afidhi Self iliyokuwa
inamkabili.
Akisoma
Mashtaka hayo Mwanasheria wa Serikali, Tumaini Kweka mbele ya Jaji,
Augustino Shangwe alisema baada ya kupitia vifungu vyote mahakama
imejiridhisha na kuona Sheikh Ponda hana hatia yoyote na kumuachia huru
tangu leo lakini katika hali ya kushangaza Sheikh Ponda amerudishwa
rumande akisubiri kesi nyingine ya madai ya uchochezi, Mkoani Morogoro
inayomkabili.
0 comments:
Post a Comment