Kufuatia kuripotiwa kwa taarifa katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusiana na mgogoro wa mpaka uliokuwepo kutokana na madai kuwa kisiwa cha Pemba ni sehemu ya Kenya, Serikali ya Tanzania imetoa taarifa rasmi kuhusiana na mgogoro huo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa Benard Membe, amewatoa hofu wananchi kuwa Pemba ni sehemu ya
Tanzania na hakuna ukweli wowote kwamba kisiwa hicho ni sehemu ya Kenya.
Akijibu kuhusiana na suala hilo Bungeni
Dodoma leo Membe amesema; “..Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
haijapata taarifa zozote rasmi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Kenya
kuhusu mgogoro wa mpaka kati ya Serikali hizi mbili… hususan madai ya
kisiwa cha Pemba kilicho ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni
sehemu ya Jamhuri ya Kenya.. Kisiwa cha Pemba ni sehemu ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na kitaendelea kubakia hivyo daima…”—Membe
“..Mara tulipopata taarifa hizi.. wizara
yangu iliwasiliana na ubalozi wetu Kenya, lakini pia tuliwasiliana na
Serikali ya Kenya yenyewe.. kucheki kama taarifa hizi zilizoandikwa
kwenye magazeti zina mshiko wa Serikali.. balozi wetu na serikali
yenyewe ya Kenya hawajui suala hili limetokea wapi…”
Kuhusiana na taarifa za kuwepo meli za
kutoka Kenya zinavyofanya shughuli za uvuvi katika eneo la Tanzania,
Membe amesema; “..nitawasiliana na wenzangu wanaohusika.. kuanzia wizara
inayohusika.. na JWTZ ambao ndio wana dhamana ya kulinda bahari yetu ya
Indian Ocean waone namna ya kudhibiti.. na namna ya kuwahakikishia
wenzetu wa Kenya kwamba hata baharini kuna mipaka yake..”– Membe
0 comments:
Post a Comment