Home » » RAIA WA TUNISIA WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS WAO

RAIA WA TUNISIA WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS WAO


Tunisians queue outside a polling station in La Marsa, Tunisia, Sunday Oct. 26, 2014.  (photo credit: AP/Hassene Dridi)
Raia wa Tunisia katika zoezi la upigaji kura

Wananchi wa Tunisia leo wanapiga kura katika uchaguzi wa kwanza wa Rais tangu kutokea vuguvugu la mapinduzi mwaka 2011.

Mapinduzi hayo yalisababisha vuguvugu hilo la mabadiliko kutabakaa katika nchi nyingine za Kiarabu.
Miongoni mwa wagombea katika kinyang'anyoro hicho ni mwanasiasa mkongwe Beji Essabsi, aliyewahi kushika nafasi muhimu wakati wa utawala kabla ya kutokea mapinduzi.

Bwana Beji Caid Essabsi anayepewa nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo ameahidi kurejeha kiwango cha juu cha utulivu wa kisiasa na kiuchumi.

Mpinzani wake wa karibu ni Rais wa mpito wa sasa Moncef Marzouki ambaye amejenga jina lake kama mpigania haki za binadamu na kama msimamizi wa moyo wa mapinduzi na anayetamani mabadiliko. Waziri wa Ulinzi wa Tunia Ghazi Jeribi amesema ana matumaini nchi itasonga mbele kidemocrasia 

Credit BBC
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger