Mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya msingi ya Kiuu Kenya amefariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kufeli somo lake la Kiswahili.
Familia ya mtoto huyo Joseph Waburi mwenye umri wa miaka kumi imesema mtoto huyo alikuwa na nidhamu ya hali ya juu.
Mama wa mwanafunzi huyo Grace Muthoni
amesema mtoto wake alienda shule Jumatatu asubuhi na aliporudi alianza
kulalamika maumivu ya kichwa na shingo, siku iliyofuatia alimpeleka
Zahanati ya Wilaya ya Nyagiti level 4
.
Siku ya pili alilazimika kumrudisha
Hospitali baada hali yake kuzidi kuwa mbaya daktari akashauri ahamishiwe
katika Zahanati ya Muran’ga Level 4 kwa matibabu zaidi wakati akisubiri
gari la wagonjwa akafariki dunia.
Mama huyo amesema uchunguzi wa awali
unaonyesha mtoto wake alipigwa na Mwalimu na kupata majeraha kichwani na
shingoni, mwili wake umehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi kubaini sababu
za kifo chake.
Mwalimu anayedaiwa kumpiga Mwanafunzi
huyo alikimbia kujificha shimoni baada ya kusikia taarifa za kifo, huku
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Joseph Mwenda akikanusha uvumi kwamba mtoto
huyo alifia shuleni.
0 comments:
Post a Comment