Home » » NYOSO NDANI MBEYA CITY WAKIIVAA AZAM KESHO CHAMANZI

NYOSO NDANI MBEYA CITY WAKIIVAA AZAM KESHO CHAMANZI

DSC_0249
KIKOSI cha timu ya Mbeya City Fc  kimefanya mazoezi ya mwisho  asubuhi ya leo tayari kwa kuivaa Azam Fc  kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara unaotarajiwa kuchezwa  Chamanzi Complex ,Mbagala,Dar Es Salaam.
Akizungumza kuelekea mchezo huo Daktari mkuu wa City, Joshua  Kaseko amesema kuwa mlinzi Yusuph Abdalah ‘Sisalo’ ataukosa mchezo huo kutokana na majeraha aliyopata  kwenye mcheo uliopita dhidi ya Ndanda Fc  na nafasi yake itazibwa na Juma Nyosso ambaye tayari amemaliza kutumikia adhabu yake  ya kutocheza mechi nane.
“Sisalo bado hali yake siyo nzuri, ni wazi hatakuwa sehemu ya kikosi kesho kwa sababu bado tunamtizamia, Juma Nyosso, amemaliza adhabu yake na kiafya yuko vizuri na imani Mwalimu Mwambusi atamjumuisha  kikosini, kucheza dhidi ya Azam kunahitaji nguvu ya ziada binafsi sina wasiwasi tena na safu ya ulinzi  baada ya urejeo wake” alisema.
DSC_0202
Katika hatua nyingine mlinzi Juma Nyosso amesema  yuko vizuri  tayari kwa  mchezo huo kwa sababu muda wote aliokuwa akitumikia adhabu alikuwa akiendelea na mazoezi.
“Niko sawa, nimekuwa nikiendelea na mazoezi muda wote niliokuwa nje ya kikosi nashukuru  hayo yamepita  na sasa niko tena  kikosini kwa ajili ya kuipigania timu yangu, nawapongeza  wenzangu  wamepambana  kwa nguvu zote  mpaka sasa tuko kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi yaliyopita si ndwele tunaganga yajayo kwa sababu huu ndiyo wakati wa kufanya kazi” alisema.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger