Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudencia Kabaka amefanikiwa kumaliza
mgomo wa madereva baada ya kutangaza kufuta agizo lililokuwa likiwataka
madereva wa mabasi na malori kwenda kusoma tena katika Chuo cha Taifa
cha Usafirishaji (NIT)
Kuhusu suala la Madereva kusoma, Serikali na Madereva wamekubaliana kukutana mwezi huu tarehe 18 kuzungumza njia mbadala ya kutumika.
Kuhusu suala la Madereva kusoma, Serikali na Madereva wamekubaliana kukutana mwezi huu tarehe 18 kuzungumza njia mbadala ya kutumika.
Miongoni mwa malalamiko ya madereva ilikuwa ni kukerwa na tochi za barabarani, hivyo jeshi la Polisi wamekubali kuziondoa.
Pia serikali imeagiza Madereva wote wapewe mikataba ya ajira za uhakika na waajiri wao na Trafiki wameagizwa kulifatilia hilo.
Hali ilikuwa mbaya kwa majira ya asubuhi ambapo abiria wa mikoani na katikati ya jiji la Dar es salaam walishindwa kupata huduma ya usafiri hali iliyosababisha abiria wa mikoani kosota katika stendi ya mabasi ya Ubungo.
Pia serikali imeagiza Madereva wote wapewe mikataba ya ajira za uhakika na waajiri wao na Trafiki wameagizwa kulifatilia hilo.
Hali ilikuwa mbaya kwa majira ya asubuhi ambapo abiria wa mikoani na katikati ya jiji la Dar es salaam walishindwa kupata huduma ya usafiri hali iliyosababisha abiria wa mikoani kosota katika stendi ya mabasi ya Ubungo.
Polisi Jijini Dar es Salaam wamelazimika kutumia mabomu ya machozi
katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo kutuliza vurugu
zinazofanywa na abiria pamoja na wananchi kufuatia mgomo wa madereva.
Shuhuda wetu ameshuhudia katika neo la Ubungo bajaji na pikipiki nazo zinalazimishwa kugoma, Dereva akileta ubishi anapigwa na usafiri wake kuharibiwa.
Umati
wa abiria wakiwa kwenye kituo cha daladala cha Darajani-Ubungo huku
kukiwa hakuna daladala yoyote inayofanya kazi baada ya kutokea kwa mgomo
wa madereva wa Daladala jijini Dar.
Baadhi
ya abiria wakiwa wamepanda magari ya mizigo baada ya kukosekana kwa
daladala maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam leo asubuhi.
Mmoja wa abiria akiongea na dereva wa kibasi kidogo kuangalia kama kuna uwezekano wa kupata usafiri maeneo ya Mwenge jijini Dar.
Katika
kituo cha mabasi cha Mpakani eneo la Mwenge zilionekana Bajaj zikipakia
na kushusha abiria baada ya madereva kuingia kwenye mgomo leo asubuhi.
Habari toka Morogoro zinaarifu kuwa Abiria wamejazana katika vituo vya daladala, bodaboda ndo zinatoa msaada (kwa wale wenye uwezo).
0 comments:
Post a Comment