Home » » KLOPP KUONDOKA DORTMUND

KLOPP KUONDOKA DORTMUND

Salim Kikeke's photo.
 
Borussia Dortmund wamethibitisha kuwa Jurgen Klopp ataondoka katika klabu hiyo ya Bundesliga mwishoni mwa msimu. Klopp, 47, ameomba kukatisha mkataba wake ambao ulikuwa unakwenda hadi mwaka 2018. Ameifundisha Dortmund tangu mwaka 2008 na kushinda makombe mawili ya ligi na kucheza fainali ya Klabu Bingwa Ulaya mwaka 2012-13. Lakini msimu huu timu hiyo ilikuwa mkiani mwezi Januari kabla ya kupanda hadi nafasi ya kumi, wakiwa pointi 37 nyuma ya Bayern Munich wanaoongoza ligi. Kocha huyo amekuwa akihusishwa na vilabu kadhaa vya England, ikiwemo Manchester United kabla ya kuteuliwa kwa Louis van Gaal, Arsenal wakati ikisuasua, na baadaye mabingwa watetezi Manchester City, ambao wamporomoka hadi nafasi ya nne, pointi 12 nyuma ya Chelsea wanaoongoza ligi.
 

 
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger