Home » » 18 WAFARIKI KATIKA AJALI YA HIACE ILIYOTOKEA MBEYA LEO

18 WAFARIKI KATIKA AJALI YA HIACE ILIYOTOKEA MBEYA LEO



 


 
Watu 18 wamefariki dunia katika ajali ya hiace maeneo ya kiwira wilayani Rungwe Mkoani Mbeya na inasemekana majeruhi ni wawili gari hii ilikuwa ikiokea mbeya mjini kwenda Tukuyu.Ajali hiyo imetokea wakati Madereva wa mabasi yaendayo Wilayani Jijini Mbeya hapa kugoma kutokana na baadhi ya mabasi kukamatwa na SUMATRA kwa makosa mbalimbali na kutakiwa kulipa faini ya Tsh 200,000 kwa kila basi jambo ambalo madereva awakufikia muhafaka na kuamua kuingia katika mgomo
Hiace hiyo iliyokuwa ikitoa huduma ya Usafiri baada ya mabasi yaendayo Wilaya za Kyela,Rungwe,Mbalali na Momba kugoma mapema leo ndipo baadhi ya daladala zikaanza kutoa huduma ya usafirishaji kwenda wilayani.Mungu Azilaze Roho za marehemu pema peponi AMEN.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger