BOTI yenye usajili wa Tanzania,
imekamatwa kwenye Bahari ya Kaskazini na baada ya kupekuliwa katika
bandari ya Arberdeen huko Scotland, imekutwa na shehena ya dawa
zakulevya.
Kwa mujibu wa mtandao wa BBC, boti hiyo inayoitwa Hamal, yenye urefu wa mita 32 na uwezo wa kubeba tani 422, ilizuiwa Alhamisi na vyombo viwili vya ulinzi vinavyofanya doria ikiwa umbali wa maili 100 kutoka usawa wa bahari mashariki mwa mji wa Arberden.
Kwa mujibu wa mtandao unaoonyesha vilipo
vyombo vya baharini, katikati ya Februari, boti hiyo ilikuwa Uturuki na
wiki mbili zilizopita ilianza safari kutoka visiwa vya Tenerife
huko Hispania na ilipokamatwa ilikuwa inaelekea Hamburg, mji wa pili kwa
ukubwa wa Ujerumani ikitazamiwa kufika usiku wa Ijumaa iliyopita.
Boti hiyo imekutwa na watu 9 wenye umri
kati ya miaka 26 na 63 na wameshtakiwa kwa kukutwa na dawa za kulevya
wakitarajiwa kupelekwa mahakamani. Hata hivyo watu hao utaifa wao
haukuweza kupatikana mara moja.
John McGowan wa mamlaka inayoshughulikia
uhalifu kitengo cha ulinzi wa mipaka (NCA-BPC), amesema boti hiyo
imekamatwa na kiwango kikubwa cha dawa za kulevya na kukamatwa kwake
kumewezekana kutokana na ushirikiano wa taasisi za ulinzi za Uingereza
na ushiriiano wa kimataifa.
“Kiasi kamili cha dawa hizo bado
hakijafahamika na upekuaji bado unaendelea kwa ushirikiano wa NCA na
Jeshi la Polisi ya Scotland,” amesema.
Chanzo:Mwanahalisi Online
0 comments:
Post a Comment