Home » » mshindi wa kura za Urais Uganda 2016 ametangazwa..

mshindi wa kura za Urais Uganda 2016 ametangazwa..


Uganda ilikua kwenye uchaguzi mkuu wa kumchagua Rais na Wabunge juzi ambapo matokeo ya awali yalianza kutolewa kuanzia jana lakini leo matokeo kamili yametolewa na Yoweri Museveni ambaye amekuwepo kwenye kiti cha Urais toka mwaka 1986 ametangazwa mshindi huku mpinzani wake mkuu ambaye ni Kizza Besigye akikataa matokeo hayo aliyoyaita ya wizi wa kura.
KTN 2
Kituo cha TV cha NBS kimeripoti kwamba huduma za Taxi mitaani, mitandao ya kijamii na huduma za benki za simu za mkononi zimerejea baada ya serikali kuamuru juzi kila kitu kizimwe kuanzia Facebook, Twitter, Whatsapp.
Rais Museveni baadae alihojiwa na kusema mitandao ya kijamii ilizimwa kwa muda mfupi tu na watu hawakutakiwa kuwa na hofu sababu ilifanywa ili kuzuia upotoshaji wa taarifa tu ambao umekua ukifanywa mara kwa mara.
Museveni 2
Rais Museveni alipokutana na Viongozi waangalizi wa uchaguzi Mzee Obasanjo na Banda nyumbani kwa Rais eneo la Rwakitura.
 
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger