Home » » MTIBWA SUGAR YAMSAJILI HASSAN DILUNGA MIAKA MIWILI

MTIBWA SUGAR YAMSAJILI HASSAN DILUNGA MIAKA MIWILI

 


Hassan Dilunga akiwa ameshika mkataba wa Mtibwa Sugar baada ya kusiani miaka miwili kuhamishia huduma zake Manungu
KIUNGO wa zamani wa Yanga SC, Hassan Dilunga amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Mtibwa Sugar ya Turiani, Manungu mkoani Morogoro. 
Kocha wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila ameiambia Bin Zubeiry Sports – Online leo kwamba, wamevutiwa kipaji cha kuzaliwa cha Dilunga ili kumsajili.
Katwila, kiungo mshambuliaji wa zamani wa Mtibwa Sugar na timu ya taifa, Taifa Stars, amesema anaamini Dilunga ni mchezaji ambaye ataisaidia timu hiyo.
Hassan Dilunga akiwa ameshika mkataba wa Mtibwa Sugar baada ya kusiani miaka miwili kuhamishia huduma zake Manungu
Dilunga anayetokea JKT Ruvu iliyoteremka Daraja baada ya msimu uliopita, ni kati ya wachezaji wawili waliosajiliwa na Mtibwa Sugar mwishoni mwa wiki, mwingine ni mshambuliaji Riffat Hamisi Msuya kutoka Ndanda FC ya Mtwara.
Na wawili hao wanafanya idadi ya wachezaji wapya waliosajiliwa Mtibwa Sugar kufika sita, baada ya awali mabingwa hao mara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, 1999 na 2000 kuwasajili kipa Shaaban Kado kutoka Mwadui, mabeki Hussein Idd kutoka Oljoro JKT, Salum Kupela Kanoni kutoka Mwadui na kiungo Suleiman Kihimb ‘Chuji’ kutoka Police Moro.
Lakini Mtibwa Sugar nayo haijaachwa salama katika dirisha hili, kwani baadhi ya wachezaji wake nao wameondoka kwenda timu nyingine, wakiwemo kipa Said Mohammed na mabeki Ally Shomary na Salim Mbonde waliohamia Simba
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger