Home » » EXCLUSIVE: Deus Kaseke kafunga usajili wa Singida United

EXCLUSIVE: Deus Kaseke kafunga usajili wa Singida United

 Baada ya headlines za muda mrefu za kocha wa Singida United mholanzi Hans van Pluijm kuonesha hisia zake kwa winga wa Yanga Deus Kaseke ambaye amewahi kumfundisha akiwa Yanga.


Usiku wa July 22 2017 club ya Singida United chini ya Mkurugenzi wa club hiyo Festo Richard Sanga imekamilisha usajili wa Deus Kaseke ambaye amemaliza mkataba wake na Yanga.





Kaseke ambaye amemaliza mkataba wake wa miaka miwili na Yanga, amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea Singida United na muda wowote kuanzia kesho atasafiri kuelekea Mwanza kuungangana na timu iliyoweka kambi.





Winga mahiri Deus Kaseke ambaye alijiunga na Yanga akitokea Mbeya City ya jijini Mbeya, ndio anakuwa mchezaji wa mwisho kukamilisha usajili wa Singida United, kwa sasa Singida wamefunga usajili wao lakini Kigi Makassi licha ya kutotangazwa lakini wamemsajili tayari.     
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger