Home » » Majambazi wawili wameuawa na Polisi Kibiti…

Majambazi wawili wameuawa na Polisi Kibiti…

 

Kupitia Taarifa ya Habari kwenye Televisheni za Tanzania leo July 20, 2017 zipo taarifa nyingi zimeripotiwa na moja kubwa ni kuhusu mapambano ya Polisi dhidi ya watu wanaosadikiwa kuwa majambazi katika operesheni maalum Kibiti, Pwani.
Taarifa hiyo ambayo imerushwa na Kituo cha Channel 10 ambapo wakati wa zoezi la kuwasaka wahalifu likiendelea Kibiti leo imeripotiwa kuwa Jeshi la Polisi limewaua watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni miongoni mwa wahalifu hao.
Mkuu wa Operation hiyo Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabaas amesema tukio hilo limetokea katika eneo la Utende lililopo Kata ya Ukwiriri Wilayani Rufiji baada ya Polisi kuwatilia shaka watu watano na walipowafuatilia walikimbia na kuwashabulia Askari kwa risasi na katika majibizano Askari walifanikiwa kuwajeruhi wawili ambao walifariki njiani wakati wanapelekwa Hospital ya Taifa Muhimbili.
>>>”Baada ya kuwasimamisha watu wale hawakusimama walikimbia na kisha kufyatua risasi hewani kuelekea walipokuwa Askari. Askari walijibu mapigo na kufanikiwa kuwajeruhi watuhumiwa wawili kati ya wale watano na wakati wanapelekwa Hospitali walipoteza maisha.” – Liberatus Sabaas.



Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger