Kocha Pep Guardiola (kushoto) akimkabidhi beki Benjamin Mendy jezi ya Manchester City baada ya kukamilisha uhamisho wake PICHA ZAIDI GONGA HAPA
KLABU
ya Manchester City ya England imefikisha jumla ya Pauni Milioni 133
ilizotumia kusajili mabeki wa pembeni, kufuatia kukamilisha uhamisho wa
Benjamin Mendy kutoka Monaco ya Ufaransa.
Mfaransa huyo anakuwa beki wa tatu wa pembeni kusajiliwa katika klabu hiyo, baada ya Kyle Walker na Danilo.
Mchezaji
huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa anajiunga na kikosi cha Pep Guardiola
kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 52 baada ya kwenda Los Angeles,
Marekani kufanyiwa vipimo vya afya na moja kwa moja kuungana na
wachezaji wenzake jana.
Beki
huyo mwenye umri wa miaka 23 amesaini mkataba wa miaka mitano na
kukabidhiwa jezi namba 22 atakayokuwa anatumia Uwanja wa Etihad na
anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza Jumatano, ambayo itakuwa ya
kirafiki dhidi ya Real Madrid mjini LA.
0 comments:
Post a Comment