Home » » JESHI LA POLISI MKOANI GEITA LIMEWAKAMATA WAGANGA WA KIENYEJI 32 WANAOPIGA RAMLI CHONGANISHI

JESHI LA POLISI MKOANI GEITA LIMEWAKAMATA WAGANGA WA KIENYEJI 32 WANAOPIGA RAMLI CHONGANISHI

Jeshi la polisi mkoa wa Geita limewakamata waganga wa kienyeji  32 wanaopiga ramli chonganishi katika msako uliofanywa hivi karibuni ili kuhakikisha mauaji ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi yanakomeshwa kabisa.

Akizunguza na waandishi wa habari baada ya kufanya msako na kuwakamata waganga hao kamanda wa polisi mkoa wa Geita  SAPC Joseph Konyo amesema wakati sasa umefika wa kuhakikisha mauaji yanayotokana na imani potofu za kishirikina yanakomeshwa na ili kuyakomesha watu wa kwanza kudhibitiwa ni waganga wa kienyeji wanaofanya shughuli zao pasipo kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa na nchi.
 
Kamanda Konyo amesema upo ushahidi wa wazi unaonyesha mahusiano ya karibu ya mauaji haya ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi na waganga wa kienyeji kwani ndio wahusika wanaoagiza viungo vya Albino na ndio hao wanaopiga ramli za uongo kuonyesha kuwa vikongwe hasa wanawake ndio wachawi.
 
Kamanda Konyo amesema serikali haiwezi kuvumilia waganga wa namna hii wanaoipotosha jamii hivyo msako huu utaendeshwa katika mikoa yote Tanzania bara ili kubaki na jamii salama isiyokuwa na vitisho vya mauaji ya kikatili kama haya.
 
Baadhi ya wananchi mkoa wa Geita wameipongeza hatua ya serikali kuanza sasa kuwachukulia hatua watuhumiwa wote wanaopatikana na tuhuma za mauaji yanayotokana na mila potofu na ushirikina.

 

Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger