MAGAZETI LEO ALHAMISI

 























 

TFF YAZINDUA JEZI MPYA TAIFA STARS,TOVUTI


Wanamitindo wakionesha jezi mpya za timu ya Taifa 'Taifa Stars'
Wanamitindo wakionesha jezi mpya za timu ya Taifa 'Taifa Stars'

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu nchini TFF leo limezindua jezi mpya za timu za Taifa, zitakazokuwa zikitumika na timu za Taifa katika michuano mbali mbali itakayokua inazikabili.
Uzinduzi huo wa jezi mpya uliofanyika katika ukumbi wa Kilimanjaro jengo la Golden Jubilee uliambatana na uziduzi wa tovuti mpya ya shirikisho, uliongozwa na mgeni rasmi Mh. Said Mtanda, mbunge wa jimbo la Mchinga na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya jamii.
Katika uzinduzi huo, kulizunduliwa jezi aina tatu, ambazo ni jezi za ugenini, jezi za nyumbani na jezi zitakazokuwa zikitumika kwa ajili ya mazoezi.
WATANZANIA SABA WATEULIWA KAMATI ZA CAF
Shirikisho la mpira barani Afrika CAF limewateua watanzania saba kuwa wajumbe wa kamati zake mbali mbali kwa kwa kipindi cha miaka miwili 2015-2017.
Walioteuliwa pamoja na kamati zao katika mabano ni:
1. Leodeger Tenga- (Makami Mwenyekiti Kamati ya Fedha, Mjumbe wa Kamati ya Uendeshaji Mashindano ya fainali za Mataifa Afrika kwa Wachezaji wa ndani (CHAN), Mwenyekiti wa Kamati ya Mpira wa Wanawake, na Mjumbe wa Kamati ya Vyama Wanachama).
2. Jamal Malinzi – (Mjumbe kamati ya Uendeshaji Mashindano ya Vijana Umri chini ya miaka 20)
3. Mwesigwa Selestine – (Mjumbe Kamati ya Uendeshaji Mashindano ya Vijana Umri chini ya Miaka 17).
4. Richard Sinamtwa -(Mjumbe Kamati ya Rufaa)
5.Dr Paul Marealle -(Mjumbe Kamati ya Tiba)
6. Lina Kessy -(Mjumbe ya Soka la Wanawake)
7. Crescentius Magori-(Mjumbe Kamati ya Soka la Ufukweni na Soka la Ndani)
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania – TFF linawapongeza wajumbe wote walioteuliwa kuingia katika kamati mbali mbali na linawatakia kila la kheri wanapoiwakilisha nchi yetu.

RAFAEL BENITEZ KOCHA MPYA REAL MADRID

 

 Salim Kikeke's photo.
Rafael Benitez ametambulishwa rasmi kama meneja mpya wa Real Madrid. Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari amesema:
"Hii ni ngumu, kutakiwa kuzungumza, lakini sijui niseme nini," amesema meneja huyo wa zamani wa Liverpool.
"Madrid ndio nyumbani. Ni hisia kali kurejea. Ni matumaini yangu kuwa mambo yatakwenda sawa, na timu icheze kandanda nzuri na kushinda makombe.
 

MBEYA CITY YABOMOLEWA TENA......MATOGORO NAYE AMFUTA JULIO NA PAUL NONGA MWADUI FC







Klabu ya Mwadui ya mkoani Shinyanga imefanikiwa kumnasa kiungo Anthony Matogola kutoka klabu ya Mbeya City.
Kiungo huyo amesaini mkataba wa mwaka mmoja leo klabuni hapo mara baada ya mazungumzo ya pande zote mbili kukamilika



PAUL NONGA AMFUATA JULIO.....AJIFUNGA MWAKA MMOJA MWADUI FC

      

 

Klabu ya Mwadui ya mkoani Shinyanga imefanikiwa kumsajili mshambuliaji Paul Nonga kutoka katika klabu ya Mbeya City kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Nonga ametua katika klabu hiyo iliyopanda daraja msimu huu kufuatia mkataba wake katika klabu ya Mbeya City kumalizika.

Akiongea na Ukurasa Wa Habari kutokea moja kwa moja mkoani Shinyanga mchana huu, Nonga amesema kikubwa zaidi ni kutafuta changamoto mpya na upande wa masirahi pia mwadui wapo vizuri. "Mimi nimefurahi kurudi nyumbani ,hii ni changamoto mpya na kingine kilichonishawishi kuja hapa ni masuala ya masirahi ,mwadui wapo vizuri "amesema Nonga

Mshambuliaji huyo ni moja ya wachezaji waanzilishi wa Mwadui Fc,aliichezea timu hiyo miaka ya nyuma wakati wanatafuta nafasi ya kupanda ligi daraja la kwanza lakini wakashindwa baada ya Rhino Rangers kuwapiku.

Baada ya hapo Nonga alihamia jkt Oljoro na baadaye Mbeya City ambapo amecheza kwa misimu miwili huku akiwa mshambuliaji tegemezi wa timu hiyo ya jijini Mbeya

Mwadui iliyopo chini ya kocha mwenye maneno mengi Jamhuri Julio Kihwelu itacheza katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu ujao mara baada ya kufanikiwa kupanda daraja msimu huu kuingia kunako ligi hiyo.

                                                         

MISWADA HII YA HABARI NI KITANZI KINGINE KWA CCM

 Reginald Mengi
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Dk. Reginald Mengi (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu mswada wa sheria ya vyombo vya habari ambao ulitaka kuwasilishwa bungeni kwa dharula.
 Mwenyekiti wa MOAT Reginald Mengi

Ukweli ni kuwa kila binadamu ana haki ya kupata maendeleo anayoyahitaji, ili kukuza na kustawisha utu wake.

Uhuru wa habari ni kati ya haki muhimu za binadamu ambazo zinatambuliwa na dunia nzima kikatiba. Watu wa habari tunaamini kwamba ‘hakuna maendeleo bila habari.’

Ukweli ni kuwa kila binadamu ana haki ya kupata maendeleo anayoyahitaji, ili kukuza na kustawisha utu wake.

Mungu alimuumba mwanadamu kwa uhuru na matakwa yake, hivyo Mungu anamshirikisha mwanadamu uhuru huo ili amtambue, amtumikie, amsifu na kumwabudu.

Kwa hivyo, kukosekana au kuminywa kwa uhuru wowote ule, uwe wa kisiasa, wa uchumi wa kuabudu (dini), kifkra, kiutamaduni na hasa uhuru wa habari, ni kuwafanya watu kuwa wendawazimu.

Kama kuna kitu mwanadamu yeyote anakipigania kwa akili zote na nguvu zote, basi ni uhuru ambao ni haki ya msingi ya kila mwanadamu.

Katiba Inayopendekezwa inasema: “ Kila mtu ana haki na uhuru wa kutafuta, kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa sahihi.

Ibara hiyo inaendelea kusema kwamba kila mtu ana uhuru wa kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji habari.

Miswada ya habari

Wakati ibara hiyo imewekwa vizuri katika katiba hiyo, miswada miwili inayokaribia kusainiwa na Rais Jakaya Kikwete inabomoa uhalisia huu.

Muswada umetengeneza mazingira magumu ya upatikanaji wa habari pamoja na usambazaji wake.

Mimi kama mwanahabari, najiuliza hivi Serikali yetu ina malengo gani na tasnia ya habari? Je, ina lengo la kuboresha au kukandamiza uhuru wa habari hasa kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu?

Nikiwa nchini Ghana, niliwahi kusoma habari za malalamiko mengi kuhusiana na miswada hii miwili ya habari.
Muswada mmoja unahusu upatikanaji wa habari na wa pili unahusu usimamizi wa vyombo vya habari. Ni kweli uhuru bila mipaka pia ni uwendawazimu.
Viongozi wa dini
Gazeti moja la kila siku lilieleza habari za viongozi wa dini hususani maaskofu wa Kanisa Katoliki na Baraza la Waislamu waliokutana, ili kujadili kadhia hiyo inayohusu uhuru wa habari nchini katika dunia hii ya ukuaji wa tasnia ya habari.
Kabla ya viongozi hawa wa dini kukutana na kujadiliana kero hii, tayari wabunge hasa wale wa upinzani walishatoa kauli zao za kutokubaliana na sheria hizo ambazo zinalenga kukandamiza uhuru wa habari nchini, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 2015.
Viongozi hao wanatamka wazi kwamba iwapo miswada hiyo itaisainiwa na Rais, nchi hii itageuka ya kidikteta kama enzi za mkoloni.
Kwa kawaida, ukiona viongozi wa dini ambao ni wasomi, wenye busara na wanaoongozwa na uchaMungu wanakutana kujadili masuala ya jamii, ujue kwamba jambo hilo Serikali imepoteza mwelekeo.
Kwa mfano, viongozi wa dini walionya mapema juu ya upungufu katika mchakato wa katiba mpya, lakini Serikali ikapuuzia; na leo matokeo yake kura ya maoni imesitishwa.
Gharama zilizotumika katika mchakato huo ni kubwa kupindukia. Wahenga wanasema: ‘asiyesikia la mkuu huvunjika guu.’
Wadau wengine wa habari wameshatoa maoni yao na kuitaka Serikali kurekebisha upungufu uliomo katika miswada hii ya habari, lakini hata hivyo Serikali inaonekana kushikilia msimamo wake.
Wamiliki wa vyombo vya habari nchini chini ya uenyekiti wa Reginad Mengi nao wametoa maoni yao na hofu yao juu, lakini je, Serikali itasikiliza vilio vya wadau hao?
Baadhi ya sheria zilizomo katika miswada hiyo hakika ni kinyume kabisa cha ukuzaji wa uhuru wa habari.
Kwa mfano, kuwadai waandishi wa habari kuwa na digrii ya kwanza kama kigezo cha kuwa mwandishi wa habari, ni kuikandamiza habari.
Je, ni kwa nini digrii ianze na waandishi na si wabunge, mawaziri au madiwani? Wakati Serikali ikiweka masharti magumu kwa waandishi wa habari, inasemekena sifa ya mtu kugombea ubunge ni kujua kusoma na kuandika.
Kibaya zaidi sheria hizi kwa nini zilingoja hadi kipindi hiki cha mwisho cha uongozi wa awamu ya nne tena kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu? Je, wananchi wapate picha gani kuhusu sheria kandamizi kama hizi?
Tafsiri ya wananchi wengi ni kwamba Serikali imeshikwa pabaya katika uchaguzi mkuu wa Oktoba, ndiyo kwa maana inakuja na sheria kandamizi kwa uhuru wa habari ili kuwanyima wananchi habari sahihi kuhusiana na uchaguzi huo.
Je, huku ndiyo kukua kwa demokrasia na utawala bora nchini Tanzania, kama tunavyojigamba katika medani za kisiasa?
Kwa upande mwingine, kama yalivyo masuala mengine ambayo yameleta migogoro katika jamii, hili nalo limeongeza mgogoro mwingine kwa serikali pamoja na wadau wa habari, wanahabari na pia viongozi wa dini.
Hivi nikisema miswada hii ni kitanzi kingine cha serikali ya CCM nitakuwa nimekosea? Je, viongozi wa dini wakiingilia kati watakuwa wameiingilia Serikali katika utendaji wake?
Viongozi wa dini wanashuhudia kwamba pole pole uhuru wa habari unapotea katika jamii yetu kwa masilahi binafsi ya wanasiasa wachache. Madhehebu ya dini yanamiliki pia vyombo vya habari, navyo vikubali kukandamizwa? Namuomba Rais Kikwete kutafakari kwa kina madhara ya kusaini miswada hii. Akumbuke kuwa hata chama chake hakiwezi kupona sheria hii ikipita.

Chanzo;MWANANCHI

UKAWA WAWAPONDA WALIOTANGAZA NIA CCM

 

 
 



Wafuasi wa Chadema wa mjini Sumbawanga, Mkoa wa Rukwa, wakiwa katika maandamano   ya kumsindikiza Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Dk Wilbroad Slaa baada ya kumaliza kuhutubia  mkutano uliofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Ndua mkoani humo. Picha na Godfrey Kahango 



    Washangaa makada kutumia fedha nyingi kwa kazi ndogo ya kutangaza nia


Sumbawanga/Dar. Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wameponda tabia ya makada wa CCM wanaotangaza nia ya kugombea urais kufanya hafla zinazotumia fedha nyingi kwenye jambo dogo.

Viongozi hao wamesema vitendo hivyo vinaonyesha kuwa chama hicho tawala hakichukii ufisadi na hivyo hakiwezi kuwa na mgombea safi.

Makada hao wamelipia muda wa matangazo ya moja kwa moja kwenye vituo vya redio na televisheni, kufanya maandalilizi ya gharama kubwa kwenye sehemu walizotangazia nia, kuandaa vipeperushi na mabango ya thamani huku baadhi wakituhumiwa kusafirisha watu kutoka sehemu mbalimbali kuhudhuria hafla hizo.

Akihutubia wakazi wa Sumbawanga mkoani Rukwa, katibu mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa alisema Serikali ya CCM ni kama ya watu wa ukoo mmoja wenye tabia zinazofanana.

Alisema Serikali imejaa tuhuma nyingi za rushwa na ufisadi na kwamba, kinachotakiwa ni kuinyima kura zote wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, mwaka huu.

Katibu huyo alisema wale wote wanaojitokeza kutangaza nia ni ‘mafisadi’ ndio maana wanatumia nguvu ya fedha kuwanunua Watanzania, jambo ambalo alisema ni kinyume cha maadili.

“Ni hatari sana kuwachagua viongozi kwa fedha, hawa wanataka kuliangamiza Taifa,” alisema.

Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema anashangaa chama kilichoasisiwa na mjamaa Mwalimu Julius Nyerere, vijana wake wanafanya sherehe kubwa kwenye jambo dogo.

“Hata mwanasiasa mkongwe Kingunge (ngombare Mwiru) anakwenda kuwa mpambe kwenye shughuli inayokiuka taratibu,” alisema na kuongeza kuwa hiyo ni ishara mbaya.

Mwenyekiti wa NLD, Emmanuel Makaidi alihoji wanaotumia fedha nyingi kwenye jambo dogo, watazirudishaje.

Alisema kama makada hao walifanya kazi halali, hawawezi kuwa na fedha zinazoweza kugharimia sherehe kubwa kama hizo.

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema mfumo mbaya wa CCM ndio unaonyesha chama hicho hakichukii mafisadi.

“Kama chama kingekuwa kinachukia ufisadi, kingeandaa utaratibu wake ili watu wote wanaotangaza nia wawe na nguvu sawa,” alisema Mbatia.

USAJILI; SIMBA YAWEWESEKA KWA MESSI

          
                 



Akizungumza kwenye makao makuu ya klabu hiyo, Msimbazi jijini Dar es Salaam, ofisa habari wa Simba, Haji Manara alisema klabu yao imeamua kumwaga mboga baada ya kuona inafanyiwa hujuma.


Dar es Salaam. Kimya kingi kina mshindo! Ndicho unachoweza kusema baada ya uongozi wa Simba kuibuka na kueleza kuwa utaishtaki Azam FC kutokana na kumshawishi kwa lengo la kumsajili Ramadhani Singano ‘Messi’ pamoja na kuponda usajili uliofanywa na wapinzani wao kwa Malimi Busungu.

Akizungumza kwenye makao makuu ya klabu hiyo, Msimbazi jijini Dar es Salaam, ofisa habari wa Simba, Haji Manara alisema klabu yao imeamua kumwaga mboga baada ya kuona inafanyiwa hujuma.

“Sisi Simba, sasa imetosha, kama watu wanaamua kumwaga ugali, sisi tunamwaga mboga, hatutaki kuyumbishwa,” alisema Manara kwa jazba huku akieleza kuwa muda wa kuyumbishwa kwa klabu yao umepita.

Hivi karibuni, Messi alihusishwa na kufanya mazungumzo ya kujiunga na Azam.

Kuhusu hilo, Manara alisema wanatafuta ushahidi ili kuishtaki klabu pinzani ambayo ilifanya mazungumzo na mchezaji huyo.

“Tumesikia kuna klabu imefanya mazungumzo na mchezaji wetu, Messi ambaye bado ana mkataba wa mwaka mmoja, kama inamtaka ije tuipe dau letu, lakini si kuitana kinyemela.

Akijibu shutuma hizo, Mtendaji Mkuu wa Azam, Saad Kawemba alikanusha madai ya kufanya mazungumzo na Messi na kueleza kuwa haina mpango wa kumsajili nyota huyo wa Simba.

Sababu za kumkosa Busungu

Simba katika mchakato wa kupata saini ya mshambuliaji Malimi Busungu wa Mgambo JKT aliyejiunga na Yanga mwishoni mwa wiki iliyopita na kumkosa.

Hata hivyo, Manara alibainisha kuwa ilimwacha nyota huyo ambaye alitaka fedha ambazo haziendani na thamani ya kiwango chake uwanjani.

“Tulimwambia ukweli Busungu kuwa kama ana nia ya kucheza Simba, dau letu ni Sh5 milioni, yeye akahitaji Sh40 milioni, fedha ambazo tulimwambia hatuwezi kumpa kwani hajafikia kiwango hicho,” alisema Manara.

Naye mwenyekiti wa kamati ya usajili wa Simba, Zacharia Hanspoppe aliwaponda Yanga kiaina baada ya kudai kuwa wao hawataki kusajili wachezaji wanaovuma, bali wanasajili kwa kuangalia mahitaji ya timu.

Alisema anajua kuwa wengi wanataka kuona Simba ikisajili wachezaji wenye majina makubwa na wanaovuma hivi sasa, lakini wao hawaangalii hilo, wanachoangalia ni ubora wa mchezaji na mahitaji ya kikosi chao kwanza.
“Sisi wala hatutaki kushindana na mtu katika kusajili, eti huyu kasajili huyu na sisi tusajili yule, hilo kwetu halipo, tunachofanya ni kusajili kulingana na timu inahitaji nini kwa wakati huo,” alisema Hanspoppe.
“Timu yetu bado ni nzuri, inakosa mambo madogo madogo, hivyo tunachofanya ni kukiongezea nguvu katika nafasi ambazo tumeona zimepwaya na wala hatutaki kusajili mchezaji kwa sababu jina lake linavuma, tunasajili mchezaji tunayemhitaji na siyo anayevuma,” alisema Hanspoppe.
Rage ahusishwa sakata la Messi
Klabu ya Simba imekuwa katika marumbano na mshambuliaji wake, Ramadhan Singano ‘Messi’ ambaye anadai kughushiwa kwa mkataba wake. “Mkataba wa Messi tumeurithi kwa uongozi uliopita (mwenyekiti alikuwa Ismail Aden Rage) na walimsajili kwa mkataba wa miaka mitatu, leo hii anadai alisaini miaka miwili. “Dole gumba na saini ni ya Messi na tulipomuuliza alisema alisainishwa na Mzee Kinesi (Joseph Itang’are), niweke wazi kuwa Simba haijawahi na haiwezi kughushi mikataba ya mchezaji yeyote,” alisema.
Alisema klabu hiyo imeunda kamati maalumu kuchunguza jambo hilo na itachukua hatua stahiki baada ya uchunguzi wao kukamilika.
Yamtupia virago Amri Kiemba
Akizungumzia usajili wa mchezaji Amri Kiemba ambaye Azam aliyokuwa akiichezea kwa mkopo imeeleza dhamira ya kumrudisha ilikomtoa (Simba), Manara alisema klabu hiyo haina mpango na mchezaji huyo.
“Hatuna mpango wa kumrudisha Kiemba, hatuna nafasi hiyo,” alisema Manara ambaye hakuwa tayari kuweka wazi kama mkataba wa mchezaji huyo na klabu hiyo umemalizika au la.
Madeni yanayoikabili klabu
“Nakiri ni kweli tunadaiwa, lakini hakuna taasisi duniani ambayo haidaiwi, hata Marekani, nchi tajiri inadaiwa, sembuse Simba, tunajipanga ili kulipa madeni hayo,” alisema Manara.
Alikiri kuwa klabu yao inadaiwa na baadhi ya wachezaji wake iliyovunja nao mikataba, Amissi Tambwe na Donald Mosoti.

Ujio wa kocha mpya na usajili
Akizungumzia kazi ya usajili na kocha mpya, Manara alisema, kocha mpya atatangazwa ndani ya siku nne kuanzia jana baada ya uongozi kukamilisha mchujo wa makocha walioomba kuinoa timu hiyo.
“Usajili tunaendelea vizuri, na kweli nilikwenda kwenye mashindano ya Cosafa (Afrika Kusini) ili kuangalia wachezaji, mchakato utakapokamilika kila kitu kitawekwa wazi, tutasajili kutokana na mahitaji yetu msimu ujao na upungufu tuliokuwa nao msimu uliopita ,” alisema.

Iyanya x Diamond - Nakupenda [Official Video]

BLATTER AJIUZULU WADHIFA WAKE FIFA

 
Sepp Blatter ameliongoza Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) kwa kipindi cha miaka 17.
Sepp Blatter ameliongoza Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) kwa kipindi cha miaka 17.

Sepp Blatter, raia wa Uswisi, ambaye alichaguliwa kwa muhula wa tano Mei 29 kuliongoza Shirikisho la Soka Duniani Fifa, ametangaza katika mkutano na waandishi wa habari Jumanne Mei 2 katika mji wa Zurich kwamba amejiuzulu kwenye wadhifa wake.
Uamzi huu unakuja kufuatia kashfa ya rushwa inayolikabili Shirikisho la Soka Dunia Fifa tangu Mei 27.
Akiwa ni mwenyekiti wa Fifa tangu mwaka 1998, Sepp Blatter ametangaza kujiuzulu Jumanne wiki hii katika mji wa Zurich, siku tano baada ya kuchaguliwa kwa muhula wa tano kama mwenyekiti wa Shirikisho hilo la kandanda Duniani.(P.T)
“ Nataka kuitisha mkutano wa dharura na kukabidhi muhula wangu kwa yoyote yule atakayeshinda katika kinyanga'nyiro cha kuwania nafasi ya mwenyekiti wa Fifa”, amesema Blatter.
Sepp Blatter na timu yake wanatuhumiwa kutoa kiholela masoko ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi na Kombe la Dunia mwaka 2022 nchini Qatar.
“ Hata kama nilichaguliwa, sikupata uungwaji mkono wa pande zote ”, amesema Blatter katika mkutano na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Fifa.
Sepp Blatter, mwenye umri wa miaka 79, amekua akishikilia wadhifa huo tangu mwaka 1998. Mswisi huyo amebaini kwamba ataitisha mkutano wa dharura kati ya mwezi Desemba mwaka 2015 na Machi mwaka 2016.
“ Ntaendelea kushikilia wadhifa wangu kwa muda wa miezi kadhaa, kabla ya kumkabidhi mwenyekiti mpya atakaye kuwa amechaguliwa", ameongeza Joseph Sepp Blatter.
Ni uamzi mzuri, kwa mujibu wa Michel Platini
Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya (Uefa), Michel Platini, amekaribisha uamzi huo wa Sepp Blatter. Lakini baadhi ya marais wa mashirikisho ya Soka kutoka mataifa ya Afrika wameshtushwa na uamzi huo, hasa Constant Omari, rais wa shirikisho la Soka la Congo, ambaye amemsifu Sepp Blatter kuwa ni mtu jasiri na mwenye uamzi.
 Na RFI
 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger