Home » » Mambo 8 yatakayofanywa katika wiki ya Simba SC

Mambo 8 yatakayofanywa katika wiki ya Simba SC

 
Jumanne August 1, 2017 Simba SC imezindua rasmi wiki ya Simba kuelekea Simba Day August 8 ambapo imekuwa kawaida kwa Klabu hiyo kuadhimisha Siku Maalumu waliyoiita ‘Simba Day’ kila ifikapo August 8 wakati ambapo timu hiyo imeweka kambi Afrika Kusini kwa ajili ya msimu ujao.
Simba SC, mbele ya waandishi wa habari akiwepo Afisa Habari wao Haji Manara na Mshirika wao wa kibiashara CEO wa EAG Group Iman Kajula wamezindua wiki ya Simba na kutaja mambo mbalimbali yatakayofanyika.
Uzinduzi huo umefanywa na timu hiyo wakiandaa mambo 8 ambayo yatafanyika ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwa watoto yatima huku Simba Day, kabla ya kucheza game ya kirafiki na Rayon Sport ya Rwanda zitachezwa mechi za utangulizi za Simba Queens dhidi ya viongozi wa Simba.
VIDEO: Manara wa Simba amefunga mjadala wa Haruna Niyonzima August 1 20
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger