Magazeti ya TZ leo July 26/2017.

 
Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo July 26 2017 kuanzia ya Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa.




























 

MAN CITY YAKAMILISHA USAJILI WA BEKI GHALI DUNIANI

 

Kocha Pep Guardiola (kushoto) akimkabidhi beki Benjamin Mendy jezi ya Manchester City baada ya kukamilisha uhamisho wake PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


USAJILI WA MABEKI WAPYA WA PEMBENI MANCHESTER CITY

Kyle Walker - Pauni Milioni 54
Benjamin Mendy - Pauni Milioni 52
Danilo - Pauni Milioni 27 
KLABU ya Manchester City ya England imefikisha jumla ya Pauni Milioni 133 ilizotumia kusajili mabeki wa pembeni, kufuatia kukamilisha uhamisho wa Benjamin Mendy kutoka Monaco ya Ufaransa.
Mfaransa huyo anakuwa beki wa tatu wa pembeni kusajiliwa katika klabu hiyo, baada ya Kyle Walker na Danilo.
Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa anajiunga na kikosi cha Pep Guardiola kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 52 baada ya kwenda Los Angeles, Marekani kufanyiwa vipimo vya afya na moja kwa moja kuungana na wachezaji wenzake jana.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 23 amesaini mkataba wa miaka mitano na kukabidhiwa jezi namba 22 atakayokuwa anatumia Uwanja wa Etihad na anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza Jumatano, ambayo itakuwa ya kirafiki dhidi ya Real Madrid mjini LA.

CHICHARITO ASAINI MIAKA MITATU WEST HAM

Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Javier Hernandez 'Chicharito' akiwa ameshika jezi ya West Ham United baada ya kukamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 16 kutoka Bayer Leverkusen ya Ujerumani akisaini mkataba wa miaka mitatu na atakuwa analipwa Pauni 140,000 kwa wiki PICHA ZAIDI GONGA HAPA 

Mtu mmoja apigwa risasi na kuuawa Mbeya.

Kwenye Magazeti ya Tanzania leo July 25, 2017 issue mbalimbali zimechukua headlines ambapo miongoni mwao ni kuhusu Mkazi mmoja wa Kyela, Mbeya Erick Mwangonda kuuawa kwa risasi na watu wasiofahamika akiwa kwenye banda lake la biashara.
Mwendesha Bajaj mkazi wa Njoro, Moshi ameuawa na mwili wake kufukiwa nyuma ya nyumba ya mtuhumiwa wa mauaji hayo wilayani Siha, Kilimanjaro.

Magazeti ya TZ leo July 25/2017

  Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo July 25 2017 kuanzia ya Udaku, Michezo na Hardnews kujionea yote makubwa yaliyoandikwa.
























Eric Bailly wa ManUnited amefungiwa na UEFA mechi 3


 
Beki wa kimataifa wa Ivory Coast anayeichezea club ya Manchester United ya England Eric Bailly leo ametangazwa kufungiwa mechi tatu na shirikisho la soka barani Ulaya UEFA baada ya kukutwa na hatia ya kosa alilolifanya katika mchezo wa Europa League.
Eric Bailly amefungiwa mechi tatu na UEFA kwa kosa lake alilolifanya katika mchezo wa UEFA Europa League wa Man United dhidi ya Celta Vigo la kumpiga usoni John Guidetti, hata hivyo Bailly kutokana na tukio hilo alioneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja.
Leo July 24 2017 UEFA wametanga kumfungia mechi tatu Bailly kutokana na kosa hilo, hivyo kutokana na adhabu hiyo aliyopewa Bailly atakosa mchezo wa Man United dhidi ya Real Madrid wa UEFA Super Cup August 8 na atakosa mchezo wa kwanza wa Champions League hiyo baada ya kukosa mchezo wa fainali ya Europa League.
HII NI VIDEO YA TUKIO LA ERIC BAILLY DHIDI YA JOHN GUIDETTI

NYOTA CHELSEA WAPOZWA KWENYE MAJI YA BWAWA SINGAPORE

 
Wachezaji wa Chelsea, Andreas Christensen, Victor Moses na Gary Cahill wakifurahia kwenye bwawa la kuogelea mjini Singapore baada ya mazoezi katika kambi yao ya kujiandaa na msimu mpya PICHA ZAIDI GONGA HAPA 

MTIBWA SUGAR YAMSAJILI HASSAN DILUNGA MIAKA MIWILI

 


Hassan Dilunga akiwa ameshika mkataba wa Mtibwa Sugar baada ya kusiani miaka miwili kuhamishia huduma zake Manungu
KIUNGO wa zamani wa Yanga SC, Hassan Dilunga amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Mtibwa Sugar ya Turiani, Manungu mkoani Morogoro. 
Kocha wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila ameiambia Bin Zubeiry Sports – Online leo kwamba, wamevutiwa kipaji cha kuzaliwa cha Dilunga ili kumsajili.
Katwila, kiungo mshambuliaji wa zamani wa Mtibwa Sugar na timu ya taifa, Taifa Stars, amesema anaamini Dilunga ni mchezaji ambaye ataisaidia timu hiyo.
Hassan Dilunga akiwa ameshika mkataba wa Mtibwa Sugar baada ya kusiani miaka miwili kuhamishia huduma zake Manungu
Dilunga anayetokea JKT Ruvu iliyoteremka Daraja baada ya msimu uliopita, ni kati ya wachezaji wawili waliosajiliwa na Mtibwa Sugar mwishoni mwa wiki, mwingine ni mshambuliaji Riffat Hamisi Msuya kutoka Ndanda FC ya Mtwara.
Na wawili hao wanafanya idadi ya wachezaji wapya waliosajiliwa Mtibwa Sugar kufika sita, baada ya awali mabingwa hao mara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, 1999 na 2000 kuwasajili kipa Shaaban Kado kutoka Mwadui, mabeki Hussein Idd kutoka Oljoro JKT, Salum Kupela Kanoni kutoka Mwadui na kiungo Suleiman Kihimb ‘Chuji’ kutoka Police Moro.
Lakini Mtibwa Sugar nayo haijaachwa salama katika dirisha hili, kwani baadhi ya wachezaji wake nao wameondoka kwenda timu nyingine, wakiwemo kipa Said Mohammed na mabeki Ally Shomary na Salim Mbonde waliohamia Simba

Makada 6 wa CHADEMA wakamatwa na Polisi wakifatilia ya Lissu

FULL VIDEO: Fatma Karume Wakili wa Lissu aongea kinachoendelea…tazama kwa kuplay video hii hapa chini!!!!

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger