Home » » Scholes amtoa Fellaini kikosini Man United

Scholes amtoa Fellaini kikosini Man United

1Paul Scholes amewatupia lawama baadhi ya wachezaji baada ya Manchester United kupoteza mchezo dhidi ya Watford kwa kufungwa mabao 3-1.
Scholes, ambaye anafanya kazi ya uchambuzi katika kituo cha runinga cha BT Sport, amedai kwamba licha ya uwepo wa majina makubwa uwanjani lakini United walionekana kucheza chini ya kiwango.
“Nadhani kwa uwezo uliooneshwa na mchezaji mmoja-mmoja uwanjani haukuwa wa kuridhisha. kwenye upande wa umiliki wa mpira ndiyo kabisa ovyo, kila mara walikuwa wakipoteza mpira.”
Moja ya wachezaji ambao Scholes amewatupia lawama sana ni Marouane Fellaini kwa namna alivyocheza kwenye eneo lake la kiungo.
“Yeah kweli nadhani Fellaini alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake; alifanya kazi yake alivyoweza,” alisema Scholes.
“Lakini kama wewe ni mtu wa Manchester United, unahitaji kuona zaidi ya alivyocheza.
“Unahitaji mtu ambaye anaweza kuzuia mashambulizi na kucheza mpira pia, mtu ambaye anaweza kudhibiti wapinzani lakini anaweza kuweka timu mabegani mwake, kusukuma timu mbele na kupiga pasi za maana kuelekea goli la wapinzani.
“Sijui kwanini Michael Carrick yupo pale halafu hachezeshwi. Awali alionekana kama anaondoka hivi lakini amebaki halafu hachezeshwi.
“Hata sijui nini kimempata.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger