Home » » MAN UNITED YANYUKWA EPL

MAN UNITED YANYUKWA EPL


WATFORD-MANUNITED                                                                                                                                                     WAKICHEZA Ugenini huko Vicarage Road Manchester United Leo wamefungwa Bao 3-1 na Watford kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
Hii ni mara ya kwanza kwa Watford kuifunga Man United katika Miaka 30.
Bao za Watford zilufungwa Dakika za 34, 83 na Penati ya Dakika ya 94 kupitia Etiene Capoye, Juan Zaniga na Troy Deeney.
Bao la Man United lilufungwa na Marcus Rashford katika Dakika ya 62.
Kwenye EPL hiki ni kipigo cha pili mfululizo kwa Man United baada ya Wikiendi iliyopita kufungwa pia na Man City lakini pia Juzi kati Wiki walichapwa 1-0 huko Rotterdam na Feyenoord kwenye Mechi yao ya kwanza ya Kundi lao la UEFA EUROPA LIGI.
Mechi inayofuata kwa Man United ni Jumatano Ugenini na Northampton ikiwa ni Mechi ya Raundi ya 3 ya EFL CUP ambalo ni Kombe la Ligi.
VIKOSI VILIVYOANZA:
Watford (3-5-2) Gomes; Cathcart, Prödl, Britos; Janmaat, Pereyra, Behrami, Capoue, Holebas; Deeney, Ighalo.
Akiba: Pantilimon, Zuniga, Kenedy, Watson, Amrabat, Guedioura, Success.
Manchester United (4-2-3-1) De Gea; Valencia, Bailly, Smalling, Shaw; Fellaini, Pogba; Rashford, Rooney, Martial; Ibrahimovic.
Akiba: Romero, Blind, Carrick, Herrera, Mata, Young, Memphis.
REFA: Michael Oliver
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger