Home » » SERIKALI YAJIVIKA MWIBA WA BVR

SERIKALI YAJIVIKA MWIBA WA BVR


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), Jenister Mhagama
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), Jenister Mhagama

PAMOJA na kazi ya uandikishaji wapiga kura katika daftari la kudumu kwa mfumo wa kielektroniki (BVR) kuambatana na kasoro lukuki, Serikali imeahidi kuwa kazi hiyo itakamilika ndani ya siku 60. 
Jenista Mhagama-Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu wa Bunge), ndiye ametoa ahadi hiyo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia hotuba ya Bajeti kwa ofisi ya waziri mkuu 2015/16.
Amesema “ndani ya siku 60 (miezi miwili), kazi hiyo itakuwa imekamilika kutokana na kuongezwa kwa mashine za BVR. Kwa sasa zipo BVR kits 4,850 na serikali inategemea kupokea zingine 3,150 ili kufikisha jumla 8,000.”
Kwa mujibu wa Mhagama, baadhi ya mikoa kama Njombe, uandikishaji tayari umekamilika.
Ameongeza kuwa, kutoka na kuwepo kwa idadi hiyo ya mashine, kuna uwezekano wa kuandikisha watu 800,000 kwa siku iwapo kila mashine moja itaweza kuandikisha watu 100.
“Iwapo mashine hizo zikitumiaka kuandikisha watu 100 kwa siku, hivyo ni wazi kuwa ndani ya siku 60 kazi ya uandikishaji katika daftari la kudumu la mpiga kura litakuwa limekamilika.
Ametaja mikoa mingine ambayo inatarajiwa kuanza kuandikishwa Mei 18 mwaka huu, kuwa ni Dodoma, Singida, Mbeya, Rukwa, Kigoma, Kagera, Katavi na Tabora.
Amesema kuwa kwa sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaendelea na uandikishaji katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Kuhusu mshauri juu ya uboreshaji wa daftari la wapiga kura na kutumia mashine za BVR, Mhagama amesema kuwa, walikataa ushauri huo kutokana na kubaini kuwa ilikuwa ni gharama kubwa zaidi.
Amefafanua kuwa, jinsi mshauri huyo kutoka Marekani alivyowashauri, ilionekana kuwa gharama ingekuwa zadi ya Sh. 321 bilioni badala ya Sh. 293 za sasa.
“Ikumbukwe kuwa uboreshaji daftari mwaka jana, uligharimu Sh. 72 bilioni na kama matumizi ya mashine ni Sh. 218 bilioni, jumla zingekuwa Sh. 321 bilioni,”amesema.
Akizungumzia uchaguzi wa Zanzibar, Mhagama amesema “masuala ya uchaguzi yatasimamiwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC). Hata hivyo, uhakika ni kwamba daftari litaboreshwa zaidi.”  
Kwa mujibu wa Mhagama, wapinzani wamekuwa wakilalamikia juu uboreshwaji wa daftari ya kudumu la wapiga kura na kuhofia uchaguzi mkuu ujao kutofanyika.
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger