Home » » MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO WAGOMA TENA LEO

MADEREVA WA VYOMBO VYA MOTO WAGOMA TENA LEO





Madereva wa Vyombo vya Usafirishaji katika maeneo mbalimbali  nchini, wameingia katika Mgomo tena leo kutotoa huduma hiyo kwa kile kinachodaiwa kwamba wanaitaka serikali iwasikilize madai ya mikataba yao kati yao na waajiri.
Hali ya mgomo huo, umepelekea adha kubwa kwa abiria wa vyombo hivyo, hasa wale waliokuwa wakielekea mikoani, pamoja na watu wenye magari yao kwani baadhi ya maeneo kama jijini Mbeya magari ya watu  binafsi yamelazimishwa kupandisha abiria tena bure na baadhi ya baiskeri ya matairi matatu hali maarufu kama bajiji na pikipiki zimeendelea kutoa huduma ya usafiri kwa bei ghari zaidi hali inayopelekea wasio na kipato kutembea kwa miguu kuelekea katika shughuri zao.
hali hii imesababisha abiria wengi wa daladala kutembea kwa miguu katika jiji hapa na baadhi ya abiri a katika stendi kuu ya mabasi jiji hapa kukosa usafiri hali inayosababisha hadha kwa abiria hao ambao wamejazana katika stendi hiyo na stendi ya nane nane hali kadhalika ni hivyo hivyo.

 


Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger