Home » » UEFA CHAMPIONS LEO; DYNAMO Vs CHELSEA: MOURINHO HAZARD KUCHEZA, PEDRO, REMY WABAKI LONDON!

UEFA CHAMPIONS LEO; DYNAMO Vs CHELSEA: MOURINHO HAZARD KUCHEZA, PEDRO, REMY WABAKI LONDON!

MOURINHO-MIMACHO


                                                                                                                                       UEFA CHAMPIONZ LIGI
MAKUNDI
Jumanne Oktoba 20
**Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku
KUNDI E
BATE Borislov v Barcelona          
Bayer Leverkusen v AS Roma                
KUNDI F
Arsenal v Bayern Munich             
Dinamo Zagreb v Olympiakos               
KUNDI G
Dynamo Kiev v Chelsea              
FC Porto v Maccabi Tel Aviv                  
KUNDI H
Valencia v KAA Gent         
Zenit Saint Petersburg v Lyon
++++++++++++++++++++++++++++++++++
JUMANNE Usiku Chelsea wapo huko Ukraine kucheza Mechi yao ya 3 ya Kundi G la UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, na Dynamo Kiev lakini Meneja wao Jose Mourinho amekataa kuthibitisha kama Staa wao Eden Hazard atacheza Mechi hiyo.
Hazard alitupwa nje kwenye Mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu England walipoichapa Aston Villa 2-0 lakini Kikosi kilichosafiri kwenda huko Ukraine hakina Mastraika Pedro na Loic Remy ambao wamebakia London kutokana na maumivu.
Licha ya mapengo hayo, Mourinho amekataa kuthibitisha kama Hazard atacheza Mechi hii ya UCL ingawa ipo nafasi kubwa lazima atapata namba.
Mechi hii na Dynamo Kiev ni muhimu mno kwa Chelsea ambao kwenye Kundi G wapo Nafasi ya 3 baada ya kushinda Mechi 1 na kufungwa 1 wakiwa na Pointi 3 huku juu yao wapo Vinara Dynamo Kiev na FC Porto ambao wote wana Pointi 4 kila mmoja.
Mourinho mwenyewe amekiri hilo aliposema: “Tunahitaji kushinda Mechi. Hatufikirii wapi tulipo, inabidi tushinde Mechi inayotukabili.”
Dynamo, wakiwa kwao Kiev, si Timu ya ubwete ingawa Ijumaa iliyopita walikumbana na kipigo chao cha kwanza katika Mechi 38 za Ligi Kuu ya Ukraine baada kupigwa 3-0 na Shakhtar Donetsk lakini kwenye Mechi zao 10 zilizopita za Ulaya wameshinda 7 na kufungwa 1 tu.
UCL-G
UEFA CHAMPIONZ LIGI
MAKUNDI
Jumatano Oktoba 21
**Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku
KUNDI A
Malmö FF v Shakhtar Donetsk              
Paris St Germain v Real Madrid             
KUNDI B
CSKA v Man United          
VfL Wolfsburg v PSV                  
KUNDI C
Atletico Madrid v FC Astana                 
Galatasaray v Benfica                 
KUNDI D
Juventus v Borussia Mönchengladbach             
Man City v Sevilla            
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger